< Zaburi 4 >
1 Kwa mwimbishaji. Kwa ala za nyuzi za muziki. Zaburi ya Daudi. Nijibu nikuitapo, Ee Mungu wangu mwenye haki! Nipumzishe katika shida zangu; nirehemu, usikie ombi langu.
“For the leader of the music; to be accompanied with stringed instruments. A psalm of David.” Hear me, when I call, O God of my righteousness! Thou hast helped me, when I was in trouble, —Have pity upon me, and hear my prayer!
2 Enyi watu, mtabadilisha utukufu wangu kuwa aibu mpaka lini? Mtapenda udanganyifu na kufuata miungu ya uongo mpaka lini?
How long, O men! will ye dishonor my dignity? How long will ye love vanity, and seek disappointment? (Pause)
3 Fahamuni hakika kwamba Bwana amewatenga wale wamchao kwa ajili yake; Bwana atanisikia nimwitapo.
Know ye that the LORD hath exalted one that is devoted to him; The LORD will hear, when I call upon him.
4 Katika hasira yako, usitende dhambi. Mkiwa vitandani mwenu, mtulie kimya mkiichunguza mioyo yenu.
Stand in awe, and sin no more; Commune with your hearts upon your beds, and desist! (Pause)
5 Toeni dhabihu zilizo haki; mtegemeeni Bwana.
Offer sacrifices of righteousness, And put your trust in the LORD!
6 Wengi wanauliza, “Ni nani awezaye kutuonyesha jema lolote?” Ee Bwana, tuangazie nuru ya uso wako.
There are many who say, Who will show us any good? LORD, lift thou up the light of thy countenance upon us!
7 Wewe umejaza moyo wangu kwa furaha kubwa kuliko watu waliopata nafaka na divai kwa wingi.
Thou puttest gladness into my heart, Greater than theirs, when their corn and wine are abundant.
8 Nitajilaza chini na kulala kwa amani, kwa kuwa wewe peke yako, Ee Bwana, waniwezesha kukaa kwa salama.
I will lay me down in peace, and sleep: For thou alone, O LORD! makest me dwell in safety.