< Zaburi 38 >

1 Zaburi ya Daudi. Maombi. Ee Bwana, usinikemee katika hasira yako, wala kuniadhibu katika ghadhabu yako.
Psalmus David, in rememorationem de sabbato. Domine, ne in furore tuo arguas me, neque in ira tua corripias me:
2 Kwa kuwa mishale yako imenichoma, na mkono wako umenishukia.
quoniam sagittæ tuæ infixæ sunt mihi, et confirmasti super me manum tuam.
3 Hakuna afya mwilini mwangu kwa sababu ya ghadhabu yako, mifupa yangu haina uzima kwa sababu ya dhambi zangu.
Non est sanitas in carne mea, a facie iræ tuæ; non est pax ossibus meis, a facie peccatorum meorum:
4 Maovu yangu yamenifunika kama mzigo usiochukulika.
quoniam iniquitates meæ supergressæ sunt caput meum, et sicut onus grave gravatæ sunt super me.
5 Majeraha yangu yameoza na yananuka, kwa sababu ya upumbavu wa dhambi zangu.
Putruerunt et corruptæ sunt cicatrices meæ, a facie insipientiæ meæ.
6 Nimeinamishwa chini na kushushwa sana, mchana kutwa nazunguka nikiomboleza.
Miser factus sum et curvatus sum usque in finem; tota die contristatus ingrediebar.
7 Viuno vyangu vimejaa maumivu yaunguzayo, hakuna afya mwilini mwangu.
Quoniam lumbi mei impleti sunt illusionibus, et non est sanitas in carne mea.
8 Nimedhoofika na kupondwa kabisa, nasononeka kwa maumivu makuu ya moyoni.
Afflictus sum, et humiliatus sum nimis; rugiebam a gemitu cordis mei.
9 Ee Bwana, yote ninayoyaonea shauku yako wazi mbele zako, kutamani kwangu sana hakufichiki mbele zako.
Domine, ante te omne desiderium meum, et gemitus meus a te non est absconditus.
10 Moyo wangu unapigapiga, nguvu zangu zimeniishia; hata macho yangu yametiwa giza.
Cor meum conturbatum est; dereliquit me virtus mea, et lumen oculorum meorum, et ipsum non est mecum.
11 Rafiki na wenzangu wananikwepa kwa sababu ya majeraha yangu; majirani zangu wanakaa mbali nami.
Amici mei et proximi mei adversum me appropinquaverunt, et steterunt; et qui juxta me erant, de longe steterunt: et vim faciebant qui quærebant animam meam.
12 Wale wanaotafuta uhai wangu wanatega mitego yao, wale ambao wangetaka kunidhuru huongea juu ya maangamizi yangu; hufanya shauri la hila mchana kutwa.
Et qui inquirebant mala mihi, locuti sunt vanitates, et dolos tota die meditabantur.
13 Mimi ni kama mtu kiziwi, asiyeweza kusikia, ni kama bubu, asiyeweza kufungua kinywa chake,
Ego autem, tamquam surdus, non audiebam; et sicut mutus non aperiens os suum.
14 nimekuwa kama mtu asiyesikia, ambaye kinywa chake hakiwezi kutoa jibu.
Et factus sum sicut homo non audiens, et non habens in ore suo redargutiones.
15 Ee Bwana, ninakungojea wewe, Ee Bwana Mungu wangu, utajibu.
Quoniam in te, Domine, speravi; tu exaudies me, Domine Deus meus.
16 Kwa kuwa nilisema, “Usiwaache wafurahie, wala wasijitukuze juu yangu mguu wangu unapoteleza.”
Quia dixi: Nequando supergaudeant mihi inimici mei; et dum commoventur pedes mei, super me magna locuti sunt.
17 Kwa maana ninakaribia kuanguka, na maumivu yangu yananiandama siku zote.
Quoniam ego in flagella paratus sum, et dolor meus in conspectu meo semper.
18 Naungama uovu wangu, ninataabishwa na dhambi yangu.
Quoniam iniquitatem meam annuntiabo, et cogitabo pro peccato meo.
19 Wengi ni wale ambao ni adui zangu hodari, wale wanaonichukia bila sababu ni wengi.
Inimici autem mei vivunt, et confirmati sunt super me: et multiplicati sunt qui oderunt me inique.
20 Wanaolipa maovu kwa wema wangu hunisingizia ninapofuata lililo jema.
Qui retribuunt mala pro bonis detrahebant mihi, quoniam sequebar bonitatem.
21 Ee Bwana, usiniache, usiwe mbali nami, Ee Mungu wangu.
Ne derelinquas me, Domine Deus meus; ne discesseris a me.
22 Ee Bwana Mwokozi wangu, uje upesi kunisaidia.
Intende in adjutorium meum, Domine Deus salutis meæ.

< Zaburi 38 >