< Zaburi 37 >

1 Zaburi ya Daudi. Usisumbuke kwa ajili ya watendao maovu, wala usiwaonee wivu watendao mabaya,
不要因作惡的人而忿怒,也不要對歹徒心生嫉妒;
2 kwa maana kama majani watanyauka mara, kama mimea ya kijani watakufa mara.
因為他們有如青草,快要枯槁,他們有如綠葉,行將零凋。
3 Mtumaini Bwana na utende yaliyo mema; Kaa katika nchi ukafurahie malisho salama.
你該信賴上主,致力善行,你必安居樂土,享受康寧。
4 Jifurahishe katika Bwana naye atakupa haja za moyo wako.
你只管在上主內喜歡,祂必滿全你心的意願。
5 Mkabidhi Bwana njia yako, mtumaini yeye, naye atatenda hili:
將你的行徑託付上主,寄望於祂,祂必使之成就。
6 Yeye atafanya haki yako ingʼae kama mapambazuko, na hukumu ya shauri lako kama jua la adhuhuri.
祂必使你的義德如光出現,祂必使你的仁義如日中天。
7 Tulia mbele za Bwana na umngojee kwa uvumilivu; usisumbuke watu wanapofanikiwa katika njia zao, wanapotekeleza mipango yao miovu.
你該在上主面前安心依靠,不要為萬事順心的人煩惱,不要因圖謀不軌的人暴燥;
8 Epuka hasira na uache ghadhabu, usihangaike: itakuongoza tu kutenda uovu.
你應控制憤恨,消除怒火,不要動怒,免得再犯罪過。
9 Kwa maana waovu watakatiliwa mbali, bali wale wanaomtumaini Bwana watairithi nchi.
因為作惡犯罪的人必被剷除;唯有仰望上主的人繼承樂土。
10 Bado kitambo kidogo, nao waovu hawataonekana, ingawa utawatafuta, hawataonekana.
惡人再過片刻,就不知所在,詳察他的住所,也不復存在。
11 Bali wanyenyekevu watairithi nchi na wafurahie amani tele.
但善人要繼承樂土,必要樂享平安幸福。
12 Waovu hula njama dhidi ya wenye haki na kuwasagia meno,
惡徒設計謀害忠義,常朝著他咬牙切齒。
13 bali Bwana huwacheka waovu, kwa sababu anajua siku yao inakuja.
上主朝著惡人發笑,因見他的日已來到。
14 Waovu huchomoa upanga na kupinda upinde, ili wawaangushe maskini na wahitaji, kuwachinja wale ambao njia zao ni nyofu.
惡人拔劍張弓,想毀滅貧困微弱的人,想屠殺操行正直的人;
15 Lakini panga zao zitachoma mioyo yao wenyewe, na pinde zao zitavunjwa.
他們的劍反刺穿他們的心肝,他們的弓將被折得破爛不堪。
16 Bora kidogo walicho nacho wenye haki kuliko wingi wa mali wa waovu wengi;
義人佔有的幸福雖少,但卻勝於惡人的富饒。
17 kwa maana nguvu za waovu zitavunjwa, lakini Bwana humtegemeza mwenye haki.
因為惡人的手臂將被折斷,義人卻有上主作支援。
18 Bwana anazifahamu siku za wanyofu, na urithi wao utadumu milele.
上主眷顧善人的歲月,他們的產業永遠常在。
19 Siku za maafa hawatanyauka, siku za njaa watafurahia wingi wa vitu.
在患難之時,他們必不蒙羞,在饑饉之日,他們必得飽飫。
20 Lakini waovu wataangamia: Adui za Bwana watakuwa kama uzuri wa mashamba, watatoweka, watatoweka kama moshi.
惡人和上主的仇人必要沉淪,像沃野的鮮花一樣凋零,必要像煙霧一般消散無影。
21 Waovu hukopa na hawalipi, bali wenye haki hutoa kwa ukarimu.
惡人借貸總不償還,義人卻常好施樂善。
22 Wale wanaobarikiwa na Bwana watairithi nchi, bali wale anaowalaani watakatiliwa mbali.
上主祝福的人將繼承福地,上主咒罵的人將被除滅跡。
23 Kama Bwana akipendezwa na njia ya mtu, yeye huimarisha hatua zake,
上主穩定善人的腳步,上主欣賞義人的道路;
24 ajapojikwaa, hataanguka, kwa maana Bwana humtegemeza kwa mkono wake.
他縱或失足,也不致顛仆,因為上主扶持著他的手。
25 Nilikuwa kijana na sasa ni mzee, lakini sijaona kamwe wenye haki wameachwa au watoto wao wakiombaomba chakula.
我作過幼童,現今已年老,從未見過正義的人被棄掉。也未見過他的後裔行乞討。
26 Wakati wote ni wakarimu na hukopesha bila masharti. Watoto wao watabarikiwa.
他既終生施惠憐恤,他的子必蒙祝福。
27 Acha ubaya na utende wema, nawe utaishi katika nchi milele.
你若避惡行善,你必存留久遠。
28 Kwa kuwa Bwana huwapenda wenye haki naye hatawaacha waaminifu wake. Watalindwa milele, lakini uzao wa waovu utakatiliwa mbali.
上主愛慕正義,必不拋棄自己的聖徒;乖戾歹徒必被消滅,惡人的子孫必被剷除。
29 Wenye haki watairithi nchi, na kuishi humo milele.
義人將要承受樂土,必在那裏永遠居住。
30 Kinywa cha mwenye haki hutamka hekima, nao ulimi wake huzungumza lililo haki.
義人的口傾吐智慧,他的舌頭講論公義。
31 Sheria ya Mungu wake imo moyoni mwake; nyayo zake hazitelezi.
天主的法律在他心田,他的腳步必堅定不偏。
32 Watu waovu huvizia wenye haki, wakitafuta kuwaua;
惡者窺伺義者,設法將他殺害;
33 lakini Bwana hatawaacha mikononi mwao wala hatawaacha wahukumiwe kuwa wakosa wanaposhtakiwa.
上主絕不將義人棄於惡人手中,上主審判時,也決不判義人受刑。
34 Mngojee Bwana, na uishike njia yake. Naye atakutukuza uirithi nchi, waovu watakapokatiliwa mbali, utaliona hilo.
你常仰望上主,遵循祂的道路:祂必要舉揚你,使你承受樂土;當祂剷除惡人時,你將欣然目睹。
35 Nimemwona mtu mwovu na mkatili akistawi kama mwerezi wa Lebanoni,
我曾見過惡人橫極一時,像茂盛的橡樹滋長不息。
36 lakini alitoweka mara na hakuonekana, ingawa nilimtafuta, hakupatikana.
當我再經過時,竟已不在眼前,我雖到處尋覓,再也沒有尋見。
37 Watafakari watu wasio na hatia, wachunguze watu wakamilifu, kuna mafanikio kwa mtu apendaye amani.
求你對正人注視,對君子觀看,愛好和平的人,子嗣必定連綿。
38 Lakini watenda dhambi wote wataangamizwa, mafanikio yao yatakatiliwa mbali.
行兇的人必盡數滅亡,惡人的後裔必全淪喪。
39 Wokovu wa wenye haki hutoka kwa Bwana, yeye ni ngome yao wakati wa shida.
義人的救護是來自上主,祂是我們困厄時的護守;
40 Bwana huwasaidia na kuwaokoa, huwaokoa kutoka kwa waovu na kuwahifadhi, kwa maana wanamkimbilia.
上主必多扶持助佑,解救他們脫離惡人,上主必予拯救,因他們曾向祂投奔

< Zaburi 37 >