< Zaburi 36 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi mtumishi wa Bwana. Kuna neno moyoni mwangu kuhusu hali ya dhambi ya mwovu. Hakuna hofu ya Mungu mbele ya macho yake.
Müzik şefi için - RAB'bin kulu Davut'un mezmuru Günah fısıldar kötü insana, Yüreğinin dibinden: Tanrı korkusu yoktur onda.
2 Kwa kuwa machoni pake mwenyewe hujisifu mno hata hawezi kugundua au kuichukia dhambi yake.
Kendini öyle beğenmiş ki, Suçunu görmez, ondan tiksinmez.
3 Maneno ya kinywa chake ni maovu na ya udanganyifu, ameacha kuwa mwenye hekima na kutenda mema.
Ağzından kötülük ve yalan akar, Akıllanmaktan, iyilik yapmaktan vazgeçmiş.
4 Hata kitandani mwake hupanga hila mbaya, hujitia katika njia ya dhambi na hakatai lililo baya.
Yatağında bile fesat düşünür, Olumsuz yolda direnir, reddetmez kötülüğü.
5 Upendo wako, Ee Bwana, unafika hadi mbinguni, uaminifu wako hadi kwenye anga.
Ya RAB, sevgin göklere, Sadakatin gökyüzüne erişir.
6 Haki yako ni kama milima mikubwa, hukumu zako ni kama kilindi kikuu. Ee Bwana, wewe huwahifadhi mwanadamu na mnyama.
Doğruluğun ulu dağlara benzer, Adaletin uçsuz bucaksız enginlere. İnsanı da, hayvanı da koruyan sensin, ya RAB.
7 Upendo wako usiokoma ni wa thamani mno! Watu wakuu na wadogo hujificha uvulini wa mbawa zako.
Sevgin ne değerli, ey Tanrı! Kanatlarının gölgesine sığınır insanoğlu.
8 Wanajifurahisha katika wingi nyumbani mwako, nawe utawanywesha katika mto wa furaha zako.
Evindeki bolluğa doyarlar, Zevklerinin ırmağından içirirsin onlara.
9 Kuwa pamoja nawe ni kijito cha uzima, katika nuru yako twaona nuru.
Çünkü yaşam kaynağı sensin, Senin ışığınla aydınlanırız.
10 Dumisha upendo wako kwa wale wanaokujua wewe, haki yako kwa wale walio wanyofu wa moyo.
Sürekli göster Seni tanıyanlara sevgini, Yüreği temiz olanlara doğruluğunu.
11 Mguu wa mwenye kiburi usije dhidi yangu, wala mkono wa mwovu usinifukuze.
Gururlunun ayağı bana varmasın, Kötülerin eli beni kovmasın.
12 Angalia jinsi watenda mabaya walivyoanguka: wametupwa chini, hawawezi kuinuka!
Kötülük yapanlar oracıkta düştüler, Yıkıldılar, kalkamazlar artık.

< Zaburi 36 >