< Zaburi 36 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi mtumishi wa Bwana. Kuna neno moyoni mwangu kuhusu hali ya dhambi ya mwovu. Hakuna hofu ya Mungu mbele ya macho yake.
برای رهبر سرایندگان. مزمور داوود، خدمتگزار خداوند. گناه در عمق دل انسان شرور لانه کرده است و هیچ ترسی از خدا ندارند.
2 Kwa kuwa machoni pake mwenyewe hujisifu mno hata hawezi kugundua au kuichukia dhambi yake.
او چنان از خود راضی است که نمی‌تواند گناهش را ببیند و از آن رویگردان شود.
3 Maneno ya kinywa chake ni maovu na ya udanganyifu, ameacha kuwa mwenye hekima na kutenda mema.
سخنانش شرارت‌آمیز و مملو از دروغ است؛ حکمت و نیکی در وجودش نیست.
4 Hata kitandani mwake hupanga hila mbaya, hujitia katika njia ya dhambi na hakatai lililo baya.
به راههای کج می‌رود و از کارهای خلاف دست نمی‌کشد.
5 Upendo wako, Ee Bwana, unafika hadi mbinguni, uaminifu wako hadi kwenye anga.
محبت تو، ای خداوند، تا به آسمانها می‌رسد و وفاداری تو به بالاتر از ابرها!
6 Haki yako ni kama milima mikubwa, hukumu zako ni kama kilindi kikuu. Ee Bwana, wewe huwahifadhi mwanadamu na mnyama.
عدالت تو همچون کوههای بزرگ پابرجاست؛ احکام تو مانند دریا عمیق است. ای خداوند، تو حافظ انسانها و حیوانات هستی.
7 Upendo wako usiokoma ni wa thamani mno! Watu wakuu na wadogo hujificha uvulini wa mbawa zako.
خدایا، محبت تو چه عظیم است! آدمیان زیر سایهٔ بالهای تو پناه می‌گیرند.
8 Wanajifurahisha katika wingi nyumbani mwako, nawe utawanywesha katika mto wa furaha zako.
آنها از برکت خانهٔ تو سیر می‌شوند و تو از چشمهٔ نیکویی خود به آنها می‌نوشانی.
9 Kuwa pamoja nawe ni kijito cha uzima, katika nuru yako twaona nuru.
تو سرچشمهٔ حیات هستی؛ از نور تو است که ما نور حیات را می‌بینیم!
10 Dumisha upendo wako kwa wale wanaokujua wewe, haki yako kwa wale walio wanyofu wa moyo.
خداوندا، محبت تو همیشه بر کسانی که تو را می‌شناسند باقی بماند و نیکویی تو پیوسته همراه راست‌دلان باشد.
11 Mguu wa mwenye kiburi usije dhidi yangu, wala mkono wa mwovu usinifukuze.
نگذار متکبران به من حمله کنند و شروران مرا متواری سازند.
12 Angalia jinsi watenda mabaya walivyoanguka: wametupwa chini, hawawezi kuinuka!
ببینید چگونه بدکاران افتاده‌اند! آنها نقش زمین شده‌اند و دیگر نمی‌توانند برخیزند!

< Zaburi 36 >