< Zaburi 36 >
1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi mtumishi wa Bwana. Kuna neno moyoni mwangu kuhusu hali ya dhambi ya mwovu. Hakuna hofu ya Mungu mbele ya macho yake.
Al maestro del coro. Di Davide servo del Signore. Nel cuore dell'empio parla il peccato, davanti ai suoi occhi non c'è timor di Dio.
2 Kwa kuwa machoni pake mwenyewe hujisifu mno hata hawezi kugundua au kuichukia dhambi yake.
Poiché egli si illude con se stesso nel ricercare la sua colpa e detestarla.
3 Maneno ya kinywa chake ni maovu na ya udanganyifu, ameacha kuwa mwenye hekima na kutenda mema.
Inique e fallaci sono le sue parole, rifiuta di capire, di compiere il bene.
4 Hata kitandani mwake hupanga hila mbaya, hujitia katika njia ya dhambi na hakatai lililo baya.
Iniquità trama sul suo giaciglio, si ostina su vie non buone, via da sé non respinge il male.
5 Upendo wako, Ee Bwana, unafika hadi mbinguni, uaminifu wako hadi kwenye anga.
Signore, la tua grazia è nel cielo, la tua fedeltà fino alle nubi;
6 Haki yako ni kama milima mikubwa, hukumu zako ni kama kilindi kikuu. Ee Bwana, wewe huwahifadhi mwanadamu na mnyama.
la tua giustizia è come i monti più alti, il tuo giudizio come il grande abisso: uomini e bestie tu salvi, Signore.
7 Upendo wako usiokoma ni wa thamani mno! Watu wakuu na wadogo hujificha uvulini wa mbawa zako.
Quanto è preziosa la tua grazia, o Dio! Si rifugiano gli uomini all'ombra delle tue ali,
8 Wanajifurahisha katika wingi nyumbani mwako, nawe utawanywesha katika mto wa furaha zako.
si saziano dell'abbondanza della tua casa e li disseti al torrente delle tue delizie.
9 Kuwa pamoja nawe ni kijito cha uzima, katika nuru yako twaona nuru.
E' in te la sorgente della vita, alla tua luce vediamo la luce.
10 Dumisha upendo wako kwa wale wanaokujua wewe, haki yako kwa wale walio wanyofu wa moyo.
Concedi la tua grazia a chi ti conosce, la tua giustizia ai retti di cuore.
11 Mguu wa mwenye kiburi usije dhidi yangu, wala mkono wa mwovu usinifukuze.
Non mi raggiunga il piede dei superbi, non mi disperda la mano degli empi.
12 Angalia jinsi watenda mabaya walivyoanguka: wametupwa chini, hawawezi kuinuka!
Ecco, sono caduti i malfattori, abbattuti, non possono rialzarsi.