< Zaburi 36 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi mtumishi wa Bwana. Kuna neno moyoni mwangu kuhusu hali ya dhambi ya mwovu. Hakuna hofu ya Mungu mbele ya macho yake.
Veisuunjohtajalle; Herran palvelijan Daavidin virsi. Synti sanoo jumalattomalle: minun sydämessäni ei ole Jumalan pelkoa hänen silmäinsä edessä.
2 Kwa kuwa machoni pake mwenyewe hujisifu mno hata hawezi kugundua au kuichukia dhambi yake.
Sillä se tekee kaiken sileäksi hänen silmissään, että hänen pahuutensa havaittaisiin ja häntä vihattaisiin.
3 Maneno ya kinywa chake ni maovu na ya udanganyifu, ameacha kuwa mwenye hekima na kutenda mema.
Hänen suunsa sanat ovat vääryyttä ja petosta; hän on lakannut tekemästä sitä, mikä taidollista ja hyvää on.
4 Hata kitandani mwake hupanga hila mbaya, hujitia katika njia ya dhambi na hakatai lililo baya.
Hän miettii turmiota vuoteessansa, hän pysyy tiellä, joka ei ole hyvä, hän ei kammo pahaa.
5 Upendo wako, Ee Bwana, unafika hadi mbinguni, uaminifu wako hadi kwenye anga.
Herra, sinun armosi ulottuu taivaisiin, sinun totuutesi pilviin asti.
6 Haki yako ni kama milima mikubwa, hukumu zako ni kama kilindi kikuu. Ee Bwana, wewe huwahifadhi mwanadamu na mnyama.
Sinun vanhurskautesi on kuin Jumalan vuoret, sinun tuomiosi niinkuin suuri syvyys, ihmistä ja eläintä sinä autat, Herra.
7 Upendo wako usiokoma ni wa thamani mno! Watu wakuu na wadogo hujificha uvulini wa mbawa zako.
Kuinka kallis on sinun armosi, Jumala! Ihmislapset etsivät sinun siipiesi suojaa.
8 Wanajifurahisha katika wingi nyumbani mwako, nawe utawanywesha katika mto wa furaha zako.
Heidät ravitaan sinun huoneesi lihavuudella, sinä annat heidän juoda suloisuutesi virrasta.
9 Kuwa pamoja nawe ni kijito cha uzima, katika nuru yako twaona nuru.
Sillä sinun tykönäsi on elämän lähde; sinun valkeudessasi me näemme valkeuden.
10 Dumisha upendo wako kwa wale wanaokujua wewe, haki yako kwa wale walio wanyofu wa moyo.
Säilytä armosi niille, jotka sinut tuntevat, ja vanhurskautesi oikeamielisille.
11 Mguu wa mwenye kiburi usije dhidi yangu, wala mkono wa mwovu usinifukuze.
Älköön ylpeyden jalka minua tallatko, älköönkä jumalattomain käsi minua karkoittako.
12 Angalia jinsi watenda mabaya walivyoanguka: wametupwa chini, hawawezi kuinuka!
Katso, pahantekijät kaatuvat, he suistuvat maahan, eivätkä voi nousta.

< Zaburi 36 >