< Zaburi 36 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi mtumishi wa Bwana. Kuna neno moyoni mwangu kuhusu hali ya dhambi ya mwovu. Hakuna hofu ya Mungu mbele ya macho yake.
To the Overseer. — By a servant of Jehovah, by David. The transgression of the wicked Is affirming within my heart, 'Fear of God is not before his eyes,
2 Kwa kuwa machoni pake mwenyewe hujisifu mno hata hawezi kugundua au kuichukia dhambi yake.
For he made [it] smooth to himself in his eyes, To find his iniquity to be hated.
3 Maneno ya kinywa chake ni maovu na ya udanganyifu, ameacha kuwa mwenye hekima na kutenda mema.
The words of his mouth [are] iniquity and deceit, He ceased to act prudently — to do good.
4 Hata kitandani mwake hupanga hila mbaya, hujitia katika njia ya dhambi na hakatai lililo baya.
Iniquity he deviseth on his bed, He stationeth himself on a way not good, Evil he doth not refuse.'
5 Upendo wako, Ee Bwana, unafika hadi mbinguni, uaminifu wako hadi kwenye anga.
O Jehovah, in the heavens [is] Thy kindness, Thy faithfulness [is] unto the clouds.
6 Haki yako ni kama milima mikubwa, hukumu zako ni kama kilindi kikuu. Ee Bwana, wewe huwahifadhi mwanadamu na mnyama.
Thy righteousness [is] as mountains of God, Thy judgments [are] a great deep. Man and beast Thou savest, O Jehovah.
7 Upendo wako usiokoma ni wa thamani mno! Watu wakuu na wadogo hujificha uvulini wa mbawa zako.
How precious [is] Thy kindness, O God, And the sons of men In the shadow of Thy wings do trust.
8 Wanajifurahisha katika wingi nyumbani mwako, nawe utawanywesha katika mto wa furaha zako.
They are filled from the fatness of Thy house, And the stream of Thy delights Thou dost cause them to drink.
9 Kuwa pamoja nawe ni kijito cha uzima, katika nuru yako twaona nuru.
For with Thee [is] a fountain of life, In Thy light we see light.
10 Dumisha upendo wako kwa wale wanaokujua wewe, haki yako kwa wale walio wanyofu wa moyo.
Draw out Thy kindness to those knowing Thee, And Thy righteousness to the upright of heart.
11 Mguu wa mwenye kiburi usije dhidi yangu, wala mkono wa mwovu usinifukuze.
Let not a foot of pride meet me, And a hand of the wicked let not move me.
12 Angalia jinsi watenda mabaya walivyoanguka: wametupwa chini, hawawezi kuinuka!
There have workers of iniquity fallen, They have been overthrown, And have not been able to arise!

< Zaburi 36 >