< Zaburi 36 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi mtumishi wa Bwana. Kuna neno moyoni mwangu kuhusu hali ya dhambi ya mwovu. Hakuna hofu ya Mungu mbele ya macho yake.
`To victorie, to Dauid, `the seruaunt of the Lord. The vniust man seide, that he trespasse in hym silf; the drede of God is not bifor hise iyen.
2 Kwa kuwa machoni pake mwenyewe hujisifu mno hata hawezi kugundua au kuichukia dhambi yake.
For he dide gilefuli in the siyt of God; that his wickidnesse be foundun to hatrede.
3 Maneno ya kinywa chake ni maovu na ya udanganyifu, ameacha kuwa mwenye hekima na kutenda mema.
The wordis of his mouth ben wickidnesse and gile, he nolde vndirstonde to do wel.
4 Hata kitandani mwake hupanga hila mbaya, hujitia katika njia ya dhambi na hakatai lililo baya.
He thouyte wickidnesse in his bed, he stood nyy al weie not good; forsothe he hatide not malice.
5 Upendo wako, Ee Bwana, unafika hadi mbinguni, uaminifu wako hadi kwenye anga.
Lord, thi merci is in heuene; and thi treuthe is `til to cloudis.
6 Haki yako ni kama milima mikubwa, hukumu zako ni kama kilindi kikuu. Ee Bwana, wewe huwahifadhi mwanadamu na mnyama.
Thi riytfulnesse is as the hillis of God; thi domes ben myche depthe of watris. Lord, thou schalt saue men and beestis;
7 Upendo wako usiokoma ni wa thamani mno! Watu wakuu na wadogo hujificha uvulini wa mbawa zako.
as thou, God, hast multiplied thi merci. But the sones of men; schulen hope in the hilyng of thi wyngis.
8 Wanajifurahisha katika wingi nyumbani mwako, nawe utawanywesha katika mto wa furaha zako.
Thei schulen be fillid gretli of the plentee of thin hows; and thou schalt yyue drynke to hem with the steef streem of thi likyng.
9 Kuwa pamoja nawe ni kijito cha uzima, katika nuru yako twaona nuru.
For the wel of life is at thee; and in thi liyt we schulen se liyt.
10 Dumisha upendo wako kwa wale wanaokujua wewe, haki yako kwa wale walio wanyofu wa moyo.
Lord, sette forth thi mercy to hem, that knowen thee; and thi ryytfulnesse to hem that ben of riytful herte.
11 Mguu wa mwenye kiburi usije dhidi yangu, wala mkono wa mwovu usinifukuze.
The foot of pryde come not to me; and the hond of the synnere moue me not.
12 Angalia jinsi watenda mabaya walivyoanguka: wametupwa chini, hawawezi kuinuka!
There thei felden doun, that worchen wickidnesse; thei ben cast out, and myyten not stonde.

< Zaburi 36 >