< Zaburi 36 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi mtumishi wa Bwana. Kuna neno moyoni mwangu kuhusu hali ya dhambi ya mwovu. Hakuna hofu ya Mungu mbele ya macho yake.
To the chief Musician, A Psalm of David the servant of the LORD. The transgression of the wicked saith within my heart, that there is no fear of God before his eyes.
2 Kwa kuwa machoni pake mwenyewe hujisifu mno hata hawezi kugundua au kuichukia dhambi yake.
For he flattereth himself in his own eyes, until his iniquity is found to be hateful.
3 Maneno ya kinywa chake ni maovu na ya udanganyifu, ameacha kuwa mwenye hekima na kutenda mema.
The words of his mouth are iniquity and deceit: he hath ceased to be wise, and to do good.
4 Hata kitandani mwake hupanga hila mbaya, hujitia katika njia ya dhambi na hakatai lililo baya.
He deviseth mischief upon his bed; he setteth himself in a way that is not good; he abhorreth not evil.
5 Upendo wako, Ee Bwana, unafika hadi mbinguni, uaminifu wako hadi kwenye anga.
Thy mercy, O LORD, is in the heavens; and thy faithfulness reacheth to the clouds.
6 Haki yako ni kama milima mikubwa, hukumu zako ni kama kilindi kikuu. Ee Bwana, wewe huwahifadhi mwanadamu na mnyama.
Thy righteousness is like the great mountains; thy judgments are a great deep: O LORD, thou preservest man and beast.
7 Upendo wako usiokoma ni wa thamani mno! Watu wakuu na wadogo hujificha uvulini wa mbawa zako.
How excellent is thy lovingkindness, O God! therefore the children of men put their trust under the shadow of thy wings.
8 Wanajifurahisha katika wingi nyumbani mwako, nawe utawanywesha katika mto wa furaha zako.
They shall be abundantly satisfied with the fatness of thy house; and thou shalt make them drink of the river of thy pleasures.
9 Kuwa pamoja nawe ni kijito cha uzima, katika nuru yako twaona nuru.
For with thee is the fountain of life: in thy light shall we see light.
10 Dumisha upendo wako kwa wale wanaokujua wewe, haki yako kwa wale walio wanyofu wa moyo.
O continue thy lovingkindness to them that know thee; and thy righteousness to the upright in heart.
11 Mguu wa mwenye kiburi usije dhidi yangu, wala mkono wa mwovu usinifukuze.
Let not the foot of pride come against me, and let not the hand of the wicked remove me.
12 Angalia jinsi watenda mabaya walivyoanguka: wametupwa chini, hawawezi kuinuka!
There are the workers of iniquity fallen: they are cast down, and shall not be able to rise.

< Zaburi 36 >