< Zaburi 36 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi mtumishi wa Bwana. Kuna neno moyoni mwangu kuhusu hali ya dhambi ya mwovu. Hakuna hofu ya Mungu mbele ya macho yake.
to/for to conduct to/for servant/slave LORD to/for David utterance transgression to/for wicked in/on/with entrails: among heart my nothing dread God to/for before eye his
2 Kwa kuwa machoni pake mwenyewe hujisifu mno hata hawezi kugundua au kuichukia dhambi yake.
for to smooth to(wards) him in/on/with eye his to/for to find iniquity: crime his to/for to hate
3 Maneno ya kinywa chake ni maovu na ya udanganyifu, ameacha kuwa mwenye hekima na kutenda mema.
word lip his evil: wickedness and deceit to cease to/for be prudent to/for be good
4 Hata kitandani mwake hupanga hila mbaya, hujitia katika njia ya dhambi na hakatai lililo baya.
evil: wickedness to devise: devise upon bed his to stand upon way: conduct not pleasant bad: evil not to reject
5 Upendo wako, Ee Bwana, unafika hadi mbinguni, uaminifu wako hadi kwenye anga.
LORD in/on/with [the] heaven kindness your faithfulness your till cloud
6 Haki yako ni kama milima mikubwa, hukumu zako ni kama kilindi kikuu. Ee Bwana, wewe huwahifadhi mwanadamu na mnyama.
righteousness your like/as mountain God (justice: judgement your *L(P)*) abyss many man and animal to save LORD
7 Upendo wako usiokoma ni wa thamani mno! Watu wakuu na wadogo hujificha uvulini wa mbawa zako.
what? precious kindness your God and son: child man in/on/with shadow wing your to seek refuge [emph?]
8 Wanajifurahisha katika wingi nyumbani mwako, nawe utawanywesha katika mto wa furaha zako.
to quench [emph?] from ashes house: home your and torrent: river delicacy your to water: drink them
9 Kuwa pamoja nawe ni kijito cha uzima, katika nuru yako twaona nuru.
for with you fountain life in/on/with light your to see: see light
10 Dumisha upendo wako kwa wale wanaokujua wewe, haki yako kwa wale walio wanyofu wa moyo.
to draw kindness your to/for to know you and righteousness your to/for upright heart
11 Mguu wa mwenye kiburi usije dhidi yangu, wala mkono wa mwovu usinifukuze.
not to come (in): come me foot pride and hand: power wicked not to wander me
12 Angalia jinsi watenda mabaya walivyoanguka: wametupwa chini, hawawezi kuinuka!
there to fall: fall to work evil: wickedness to thrust and not be able to arise: rise

< Zaburi 36 >