< Zaburi 36 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi mtumishi wa Bwana. Kuna neno moyoni mwangu kuhusu hali ya dhambi ya mwovu. Hakuna hofu ya Mungu mbele ya macho yake.
“For the leader of the music. A psalm of David, the servant of the Lord.” To speak of the ungodliness of the wicked is in my heart. He hath no fear of God before his eyes.
2 Kwa kuwa machoni pake mwenyewe hujisifu mno hata hawezi kugundua au kuichukia dhambi yake.
For he flattereth himself in his own eyes, Till his iniquity is found out and hated.
3 Maneno ya kinywa chake ni maovu na ya udanganyifu, ameacha kuwa mwenye hekima na kutenda mema.
The words of his mouth are iniquity and deceit; He neglecteth to be wise and to do good.
4 Hata kitandani mwake hupanga hila mbaya, hujitia katika njia ya dhambi na hakatai lililo baya.
He deviseth mischief upon his bed; He persevereth in an evil way; He abhorreth not sin.
5 Upendo wako, Ee Bwana, unafika hadi mbinguni, uaminifu wako hadi kwenye anga.
Thy goodness, O LORD! reacheth to the heavens, And thy faithfulness to the clouds;
6 Haki yako ni kama milima mikubwa, hukumu zako ni kama kilindi kikuu. Ee Bwana, wewe huwahifadhi mwanadamu na mnyama.
Thy righteousness is like the high mountains; Thy judgments are a great deep; Thou, O LORD! preservest man and beast!
7 Upendo wako usiokoma ni wa thamani mno! Watu wakuu na wadogo hujificha uvulini wa mbawa zako.
How precious is thy loving-kindness, O God! Yea, the sons of men seek refuge under the shadow of thy wings.
8 Wanajifurahisha katika wingi nyumbani mwako, nawe utawanywesha katika mto wa furaha zako.
They are satisfied with the abundance of thy house, And thou causest them to drink of the full stream of thy pleasures.
9 Kuwa pamoja nawe ni kijito cha uzima, katika nuru yako twaona nuru.
For with thee is the fountain of life; Through thy light we see light.
10 Dumisha upendo wako kwa wale wanaokujua wewe, haki yako kwa wale walio wanyofu wa moyo.
O continue thy loving-kindness to them that know thee, And thy favor to the upright in heart!
11 Mguu wa mwenye kiburi usije dhidi yangu, wala mkono wa mwovu usinifukuze.
Let not the foot of the proud come upon me, Nor the hand of the wicked remove me!
12 Angalia jinsi watenda mabaya walivyoanguka: wametupwa chini, hawawezi kuinuka!
Lo! already are the workers of iniquity fallen; They are cast down; they are unable to rise!

< Zaburi 36 >