< Zaburi 36 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi mtumishi wa Bwana. Kuna neno moyoni mwangu kuhusu hali ya dhambi ya mwovu. Hakuna hofu ya Mungu mbele ya macho yake.
The transgression of the wicked says within my heart, that there is no fear of God before his eyes.
2 Kwa kuwa machoni pake mwenyewe hujisifu mno hata hawezi kugundua au kuichukia dhambi yake.
For he flatters himself in his own eyes, until his iniquity be found to be hateful.
3 Maneno ya kinywa chake ni maovu na ya udanganyifu, ameacha kuwa mwenye hekima na kutenda mema.
The words of his mouth are iniquity and deceit: he has left off to be wise, and to do good.
4 Hata kitandani mwake hupanga hila mbaya, hujitia katika njia ya dhambi na hakatai lililo baya.
He devises mischief on his bed; he sets himself in a way that is not good; he abhors not evil.
5 Upendo wako, Ee Bwana, unafika hadi mbinguni, uaminifu wako hadi kwenye anga.
Your mercy, O LORD, is in the heavens; and your faithfulness reaches to the clouds.
6 Haki yako ni kama milima mikubwa, hukumu zako ni kama kilindi kikuu. Ee Bwana, wewe huwahifadhi mwanadamu na mnyama.
Your righteousness is like the great mountains; your judgments are a great deep: O LORD, you preserve man and beast.
7 Upendo wako usiokoma ni wa thamani mno! Watu wakuu na wadogo hujificha uvulini wa mbawa zako.
How excellent is your loving kindness, O God! therefore the children of men put their trust under the shadow of your wings.
8 Wanajifurahisha katika wingi nyumbani mwako, nawe utawanywesha katika mto wa furaha zako.
They shall be abundantly satisfied with the fatness of your house; and you shall make them drink of the river of your pleasures.
9 Kuwa pamoja nawe ni kijito cha uzima, katika nuru yako twaona nuru.
For with you is the fountain of life: in your light shall we see light.
10 Dumisha upendo wako kwa wale wanaokujua wewe, haki yako kwa wale walio wanyofu wa moyo.
O continue your loving kindness to them that know you; and your righteousness to the upright in heart.
11 Mguu wa mwenye kiburi usije dhidi yangu, wala mkono wa mwovu usinifukuze.
Let not the foot of pride come against me, and let not the hand of the wicked remove me.
12 Angalia jinsi watenda mabaya walivyoanguka: wametupwa chini, hawawezi kuinuka!
There are the workers of iniquity fallen: they are cast down, and shall not be able to rise.

< Zaburi 36 >