< Zaburi 36 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi mtumishi wa Bwana. Kuna neno moyoni mwangu kuhusu hali ya dhambi ya mwovu. Hakuna hofu ya Mungu mbele ya macho yake.
For the Leader. A Psalm of David the servant of the LORD. Transgression speaketh to the wicked, methinks — there is no fear of God before his eyes.
2 Kwa kuwa machoni pake mwenyewe hujisifu mno hata hawezi kugundua au kuichukia dhambi yake.
For it flattereth him in his eyes, until his iniquity be found, and he be hated.
3 Maneno ya kinywa chake ni maovu na ya udanganyifu, ameacha kuwa mwenye hekima na kutenda mema.
The words of his mouth are iniquity and deceit; he hath left off to be wise, to do good.
4 Hata kitandani mwake hupanga hila mbaya, hujitia katika njia ya dhambi na hakatai lililo baya.
He deviseth iniquity upon his bed; he setteth himself in a way that is not good; he abhorreth not evil.
5 Upendo wako, Ee Bwana, unafika hadi mbinguni, uaminifu wako hadi kwenye anga.
Thy lovingkindness, O LORD, is in the heavens; Thy faithfulness reacheth unto the skies.
6 Haki yako ni kama milima mikubwa, hukumu zako ni kama kilindi kikuu. Ee Bwana, wewe huwahifadhi mwanadamu na mnyama.
Thy righteousness is like the mighty mountains; Thy judgments are like the great deep; man and beast Thou preservest, O LORD.
7 Upendo wako usiokoma ni wa thamani mno! Watu wakuu na wadogo hujificha uvulini wa mbawa zako.
How precious is Thy lovingkindness, O God! and the children of men take refuge in the shadow of Thy wings.
8 Wanajifurahisha katika wingi nyumbani mwako, nawe utawanywesha katika mto wa furaha zako.
They are abundantly satisfied with the fatness of Thy house; and Thou makest them drink of the river of Thy pleasures.
9 Kuwa pamoja nawe ni kijito cha uzima, katika nuru yako twaona nuru.
For with Thee is the fountain of life; in Thy light do we see light.
10 Dumisha upendo wako kwa wale wanaokujua wewe, haki yako kwa wale walio wanyofu wa moyo.
O continue Thy lovingkindness unto them that know Thee; and Thy righteousness to the upright in heart.
11 Mguu wa mwenye kiburi usije dhidi yangu, wala mkono wa mwovu usinifukuze.
Let not the foot of pride overtake me, and let not the hand of the wicked drive me away.
12 Angalia jinsi watenda mabaya walivyoanguka: wametupwa chini, hawawezi kuinuka!
There are the workers of iniquity fallen; they are thrust down, and are not able to rise.

< Zaburi 36 >