< Zaburi 36 >
1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi mtumishi wa Bwana. Kuna neno moyoni mwangu kuhusu hali ya dhambi ya mwovu. Hakuna hofu ya Mungu mbele ya macho yake.
For the choirmaster. A Psalm of David, the servant of the LORD. An oracle is in my heart regarding the transgression of the wicked man: There is no fear of God before his eyes.
2 Kwa kuwa machoni pake mwenyewe hujisifu mno hata hawezi kugundua au kuichukia dhambi yake.
For his eyes are too full of conceit to detect or hate his own sin.
3 Maneno ya kinywa chake ni maovu na ya udanganyifu, ameacha kuwa mwenye hekima na kutenda mema.
The words of his mouth are wicked and deceitful; he has ceased to be wise and well-doing.
4 Hata kitandani mwake hupanga hila mbaya, hujitia katika njia ya dhambi na hakatai lililo baya.
Even on his bed he plots wickedness; he sets himself on a path that is not good; he fails to reject evil.
5 Upendo wako, Ee Bwana, unafika hadi mbinguni, uaminifu wako hadi kwenye anga.
Your loving devotion, O LORD, reaches to the heavens, Your faithfulness to the clouds.
6 Haki yako ni kama milima mikubwa, hukumu zako ni kama kilindi kikuu. Ee Bwana, wewe huwahifadhi mwanadamu na mnyama.
Your righteousness is like the highest mountains; Your judgments are like the deepest sea. O LORD, You preserve man and beast.
7 Upendo wako usiokoma ni wa thamani mno! Watu wakuu na wadogo hujificha uvulini wa mbawa zako.
How precious is Your loving devotion, O God, that the children of men take refuge in the shadow of Your wings!
8 Wanajifurahisha katika wingi nyumbani mwako, nawe utawanywesha katika mto wa furaha zako.
They feast on the abundance of Your house, and You give them drink from Your river of delights.
9 Kuwa pamoja nawe ni kijito cha uzima, katika nuru yako twaona nuru.
For with You is the fountain of life; in Your light we see light.
10 Dumisha upendo wako kwa wale wanaokujua wewe, haki yako kwa wale walio wanyofu wa moyo.
Extend Your loving devotion to those who know You, and Your righteousness to the upright in heart.
11 Mguu wa mwenye kiburi usije dhidi yangu, wala mkono wa mwovu usinifukuze.
Let not the foot of the proud come against me, nor the hand of the wicked drive me away.
12 Angalia jinsi watenda mabaya walivyoanguka: wametupwa chini, hawawezi kuinuka!
There the evildoers lie fallen, thrown down and unable to rise.