< Zaburi 36 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi mtumishi wa Bwana. Kuna neno moyoni mwangu kuhusu hali ya dhambi ya mwovu. Hakuna hofu ya Mungu mbele ya macho yake.
For the Chief Musician. By David, the servant of the LORD. A revelation is within my heart about the disobedience of the wicked: There is no fear of God before his eyes.
2 Kwa kuwa machoni pake mwenyewe hujisifu mno hata hawezi kugundua au kuichukia dhambi yake.
For he flatters himself in his own eyes, too much to detect and hate his sin.
3 Maneno ya kinywa chake ni maovu na ya udanganyifu, ameacha kuwa mwenye hekima na kutenda mema.
The words of his mouth are iniquity and deceit. He has ceased to be wise and to do good.
4 Hata kitandani mwake hupanga hila mbaya, hujitia katika njia ya dhambi na hakatai lililo baya.
He plots iniquity on his bed. He sets himself in a way that is not good. He does not abhor evil.
5 Upendo wako, Ee Bwana, unafika hadi mbinguni, uaminifu wako hadi kwenye anga.
Your loving kindness, LORD, is in the heavens. Your faithfulness reaches to the skies.
6 Haki yako ni kama milima mikubwa, hukumu zako ni kama kilindi kikuu. Ee Bwana, wewe huwahifadhi mwanadamu na mnyama.
Your righteousness is like the mountains of God. Your judgments are like a great deep. LORD, you preserve man and animal.
7 Upendo wako usiokoma ni wa thamani mno! Watu wakuu na wadogo hujificha uvulini wa mbawa zako.
How precious is your loving kindness, God! The children of men take refuge under the shadow of your wings.
8 Wanajifurahisha katika wingi nyumbani mwako, nawe utawanywesha katika mto wa furaha zako.
They shall be abundantly satisfied with the abundance of your house. You will make them drink of the river of your pleasures.
9 Kuwa pamoja nawe ni kijito cha uzima, katika nuru yako twaona nuru.
For with you is the spring of life. In your light we will see light.
10 Dumisha upendo wako kwa wale wanaokujua wewe, haki yako kwa wale walio wanyofu wa moyo.
Oh continue your loving kindness to those who know you, your righteousness to the upright in heart.
11 Mguu wa mwenye kiburi usije dhidi yangu, wala mkono wa mwovu usinifukuze.
Do not let the foot of pride come against me. Do not let the hand of the wicked drive me away.
12 Angalia jinsi watenda mabaya walivyoanguka: wametupwa chini, hawawezi kuinuka!
There the workers of iniquity are fallen. They are thrust down, and shall not be able to rise.

< Zaburi 36 >