< Zaburi 36 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi mtumishi wa Bwana. Kuna neno moyoni mwangu kuhusu hali ya dhambi ya mwovu. Hakuna hofu ya Mungu mbele ya macho yake.
Zborovođi. Od sluge Jahvina Davida. Grešan je naum u srcu zlotvora, straha Božjega nema on pred očima.
2 Kwa kuwa machoni pake mwenyewe hujisifu mno hata hawezi kugundua au kuichukia dhambi yake.
Sam sebi on laska suviše, grijeha svog ne vidi i ne mrzi.
3 Maneno ya kinywa chake ni maovu na ya udanganyifu, ameacha kuwa mwenye hekima na kutenda mema.
Riječi usta njegovih prijevara su i zlodjelo, za razumnost i dobro on više ne mari.
4 Hata kitandani mwake hupanga hila mbaya, hujitia katika njia ya dhambi na hakatai lililo baya.
Bezakonje smišlja na postelji svojoj, na opaku ostaje putu, od zla ne odustaje.
5 Upendo wako, Ee Bwana, unafika hadi mbinguni, uaminifu wako hadi kwenye anga.
Do neba je, Jahve, dobrota tvoja, do oblaka vjernost tvoja.
6 Haki yako ni kama milima mikubwa, hukumu zako ni kama kilindi kikuu. Ee Bwana, wewe huwahifadhi mwanadamu na mnyama.
Pravednost je tvoja k'o Božji vrhunci, a sudovi tvoji k'o duboko more: ljude i stoku ti, Jahve, spasavaš.
7 Upendo wako usiokoma ni wa thamani mno! Watu wakuu na wadogo hujificha uvulini wa mbawa zako.
Kako li je dragocjena, Bože, dobrota tvoja, pod sjenu krila tvojih ljudi se sklanjaju;
8 Wanajifurahisha katika wingi nyumbani mwako, nawe utawanywesha katika mto wa furaha zako.
site se pretilinom Doma tvojega, potocima svojih slasti ti ih napajaš.
9 Kuwa pamoja nawe ni kijito cha uzima, katika nuru yako twaona nuru.
U tebi je izvor životni, tvojom svjetlošću mi svjetlost vidimo.
10 Dumisha upendo wako kwa wale wanaokujua wewe, haki yako kwa wale walio wanyofu wa moyo.
Zakrili dobrotom sve koji te štuju i pravednošću svojom sve koji su srca čestita.
11 Mguu wa mwenye kiburi usije dhidi yangu, wala mkono wa mwovu usinifukuze.
Neka me ne zgazi noga ohola, i ruka grešnika neka me ne goni.
12 Angalia jinsi watenda mabaya walivyoanguka: wametupwa chini, hawawezi kuinuka!
Gle, padoše koji čine bezakonje: oboreni su da više ne ustanu.

< Zaburi 36 >