< Zaburi 36 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi mtumishi wa Bwana. Kuna neno moyoni mwangu kuhusu hali ya dhambi ya mwovu. Hakuna hofu ya Mungu mbele ya macho yake.
耶和華的僕人大衛的詩,交與伶長。 惡人的罪過在他心裏說: 我眼中不怕上帝!
2 Kwa kuwa machoni pake mwenyewe hujisifu mno hata hawezi kugundua au kuichukia dhambi yake.
他自誇自媚, 以為他的罪孽終不顯露,不被恨惡。
3 Maneno ya kinywa chake ni maovu na ya udanganyifu, ameacha kuwa mwenye hekima na kutenda mema.
他口中的言語盡是罪孽詭詐; 他與智慧善行已經斷絕。
4 Hata kitandani mwake hupanga hila mbaya, hujitia katika njia ya dhambi na hakatai lililo baya.
他在床上圖謀罪孽, 定意行不善的道,不憎惡惡事。
5 Upendo wako, Ee Bwana, unafika hadi mbinguni, uaminifu wako hadi kwenye anga.
耶和華啊,你的慈愛上及諸天; 你的信實達到穹蒼。
6 Haki yako ni kama milima mikubwa, hukumu zako ni kama kilindi kikuu. Ee Bwana, wewe huwahifadhi mwanadamu na mnyama.
你的公義好像高山; 你的判斷如同深淵。 耶和華啊,人民、牲畜,你都救護。
7 Upendo wako usiokoma ni wa thamani mno! Watu wakuu na wadogo hujificha uvulini wa mbawa zako.
上帝啊,你的慈愛何其寶貴! 世人投靠在你翅膀的蔭下。
8 Wanajifurahisha katika wingi nyumbani mwako, nawe utawanywesha katika mto wa furaha zako.
他們必因你殿裏的肥甘得以飽足; 你也必叫他們喝你樂河的水。
9 Kuwa pamoja nawe ni kijito cha uzima, katika nuru yako twaona nuru.
因為,在你那裏有生命的源頭; 在你的光中,我們必得見光。
10 Dumisha upendo wako kwa wale wanaokujua wewe, haki yako kwa wale walio wanyofu wa moyo.
願你常施慈愛給認識你的人, 常以公義待心裏正直的人。
11 Mguu wa mwenye kiburi usije dhidi yangu, wala mkono wa mwovu usinifukuze.
不容驕傲人的腳踐踏我; 不容凶惡人的手趕逐我。
12 Angalia jinsi watenda mabaya walivyoanguka: wametupwa chini, hawawezi kuinuka!
在那裏,作孽的人已經仆倒; 他們被推倒,不能再起來。

< Zaburi 36 >