< Zaburi 35 >
1 Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, pingana na wale wanaopingana nami, upigane na hao wanaopigana nami.
Pleiteia, Senhor, com aqueles que pleiteiam comigo: peleja contra os que pelejam contra mim.
2 Chukua ngao na kigao. Inuka unisaidie.
Pega do escudo e da rodela, e levanta-te em minha ajuda.
3 Inua mkuki wako na fumo lako dhidi ya hao wanaonifuatia. Iambie nafsi yangu, “Mimi ni wokovu wako.”
Tira da lança e obstroi o caminho aos que me perseguem; dize à minha alma: Eu sou a tua salvação.
4 Wafedheheshwe na waaibishwe wale wanaotafuta uhai wangu. Wanaofanya shauri kuniangamiza warudishwe nyuma kwa hofu.
Sejam confundidos e envergonhados os que buscam a minha vida: voltem atráz e envergonhem-se os que contra mim tentam mal.
5 Wawe kama makapi yapeperushwayo na upepo, malaika wa Bwana akiwafukuza.
Sejam como moinho perante o vento, o anjo do Senhor os faça fugir.
6 Njia yao na iwe giza na ya utelezi, malaika wa Bwana akiwafuatilia.
Seja o seu caminho tenebroso e escorregadio, e o anjo do Senhor os persiga.
7 Kwa vile walinifichia wavu wao bila sababu, na bila sababu wamenichimbia shimo,
Porque sem causa encobriram de mim a rede na cova, a qual sem razão cavaram para a minha alma.
8 maafa na yawapate ghafula: wavu walionifichia na uwatege wenyewe, na waanguke katika shimo hilo, kwa maangamizo yao.
Sobrevenha-lhe destruição sem o saber, e prenda-o a rede que ocultou; caia ele nessa mesma destruição.
9 Ndipo nafsi yangu itashangilia katika Bwana na kuufurahia wokovu wake.
E a minha alma se alegrará no Senhor; alegrar-se-á na sua salvação.
10 Nitapaza sauti yangu nikisema, “Ni nani aliye kama wewe, Ee Bwana? Wewe huwaokoa maskini kutokana na wale walio na nguvu kuliko wao, maskini na mhitaji kutokana na wanaowanyangʼanya!”
Todos os meus ossos dirão: Senhor, quem é como tu, que livras o pobre daquele que é mais forte do que ele? sim, o pobre e o necessitado daquele que o rouba.
11 Mashahidi wakatili wanainuka, wananiuliza mambo nisiyoyajua.
Falsas testemunhas se levantaram: depuzeram contra mim coisas que eu não sabia.
12 Wananilipa baya kwa jema na kuiacha nafsi yangu ukiwa.
Tornaram-me o mal pelo bem, roubando a minha alma.
13 Lakini walipokuwa wagonjwa, nilivaa nguo ya gunia na nikajinyenyekesha kwa kufunga. Maombi yangu yaliponirudia bila kujibiwa,
Mas, quanto a mim, quando estavam enfermos, o meu vestido era o saco; humilhava a minha alma com o jejum, e a minha oração voltava para o meu seio.
14 niliendelea kuomboleza kama vile wao ni rafiki au ndugu. Niliinamisha kichwa chini kwa huzuni kama ninayemwombolezea mama yangu.
Portava-me como se ele fôra meu irmão ou amigo; andava lamentando e muito encurvado, como quem chora por sua mãe.
15 Lakini nilipojikwaa, walikusanyika kwa shangwe; washambuliaji walijikusanya dhidi yangu bila mimi kujua. Walinisingizia pasipo kukoma.
Mas eles com a minha adversidade se alegravam e se congregavam: os objetos se congregavam contra mim, e eu não o sabia; rasgavam-me, e não cessavam.
16 Kama watu wasiomcha Mungu, wamenidhihaki, wamenisagia meno.
Como hipócritas zombadores nas festas, rangiam os dentes contra mim.
17 Ee Bwana, utatazama mpaka lini? Niokoe maisha yangu na maangamizi yao, uhai wangu wa thamani kutokana na simba hawa.
Senhor, até quando verás isto? resgata a minha alma das suas assolações, e a minha predileta dos leões,
18 Nami nitakushukuru mbele ya kusanyiko kubwa, nitakusifu katikati ya watu wengi.
Louvar-te-ei na grande congregação: entre muitíssimo povo te celebrarei.
19 Usiwaache wale wanaonisimanga, wale ambao ni adui zangu bila sababu; usiwaache wale ambao ni adui zangu bila sababu wakonyeze jicho kwa hila.
Não se alegrem os meus inimigos de mim sem razão, nem acenem com os olhos aqueles que me aborrecem sem causa.
20 Hawazungumzi kwa amani, bali wanatunga mashtaka ya uongo dhidi ya wale wanaoishi kwa utulivu katika nchi.
Pois não falam de paz; antes projetam enganar os quietos da terra.
21 Hunifumbulia vinywa vyao wakisema, “Aha! Aha! Kwa macho yetu wenyewe tumeliona.”
Abrem a boca de par em par contra mim, e dizem: Ólá, Ólá! os nossos olhos o viram.
22 Ee Bwana, umeona hili, usiwe kimya. Usiwe mbali nami, Ee Bwana.
Tu, Senhor, o tens visto, não te cales: Senhor, não te alongues de mim;
23 Amka, inuka unitetee! Unipiganie Mungu wangu na Bwana wangu.
Desperta e acorda para o meu julgamento, para a minha causa, Deus meu, e Senhor meu.
24 Nihukumu kwa haki yako, Ee Bwana Mungu wangu, sawasawa na haki yako; usiwaache wakusimange.
Julga-me segundo a tua justiça, Senhor Deus meu, e não deixes que se alegrem de mim.
25 Usiwaache wafikiri, “Aha, hili ndilo tulilotaka!” Au waseme, “Tumemmeza.”
Não digam em seus corações: Eia, sus, alma nossa: não digam: Nós o havemos devorado.
26 Wote wanaofurahia dhiki yangu waaibishwe na wachanganyikiwe; hao wanaojiinua dhidi yangu wavikwe aibu na dharau.
Envergonhem-se e confundam-se à uma os que se alegram com o meu mal; vistam-se de vergonha e de confusão os que se engrandecem contra mim.
27 Wale wanaofurahia hukumu yangu ya haki wapige kelele za shangwe na furaha; hebu waseme siku zote, “Bwana atukuzwe, ambaye amefurahia mafanikio ya mtumishi wake.”
Cantem e alegrem-se os que amam a minha justiça, e digam continuamente: O Senhor seja engrandecido, o qual ama a prosperidade do seu servo.
28 Ulimi wangu utanena haki yako na sifa zako mchana kutwa.
E assim a minha língua falará da tua justiça e do teu louvor todo o dia.