< Zaburi 35 >

1 Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, pingana na wale wanaopingana nami, upigane na hao wanaopigana nami.
Davidov. Optuži, Jahve, tužitelje moje i napadni one koji mene napadaju!
2 Chukua ngao na kigao. Inuka unisaidie.
Stavi oklop, uzmi štit svoj i ustani meni u pomoć!
3 Inua mkuki wako na fumo lako dhidi ya hao wanaonifuatia. Iambie nafsi yangu, “Mimi ni wokovu wako.”
Zavitlaj kopljem i presretni progonitelje moje, reci mojoj duši: “Ja sam tvoje spasenje.”
4 Wafedheheshwe na waaibishwe wale wanaotafuta uhai wangu. Wanaofanya shauri kuniangamiza warudishwe nyuma kwa hofu.
Nek' se smetu i postide koji život moj traže, nek' uzmaknu i nek' se posrame koji mi propast snuju!
5 Wawe kama makapi yapeperushwayo na upepo, malaika wa Bwana akiwafukuza.
Nek' budu k'o pljeva na vjetru kad ih Anđeo Jahvin potjera!
6 Njia yao na iwe giza na ya utelezi, malaika wa Bwana akiwafuatilia.
Mračni i skliski bili im putovi kad ih Anđeo Jahvin bude gonio!
7 Kwa vile walinifichia wavu wao bila sababu, na bila sababu wamenichimbia shimo,
Bez razloga napeše mi mrežu, bez razloga grob duši mojoj iskopaše.
8 maafa na yawapate ghafula: wavu walionifichia na uwatege wenyewe, na waanguke katika shimo hilo, kwa maangamizo yao.
Propast će ih stići iznenada, u mrežu koju napeše sami će se uhvatiti, past će u jamu što je iskopaše!
9 Ndipo nafsi yangu itashangilia katika Bwana na kuufurahia wokovu wake.
A moja će duše klicati u Jahvi, radovat će se u spasenju njegovu.
10 Nitapaza sauti yangu nikisema, “Ni nani aliye kama wewe, Ee Bwana? Wewe huwaokoa maskini kutokana na wale walio na nguvu kuliko wao, maskini na mhitaji kutokana na wanaowanyangʼanya!”
Sve će kosti moje govoriti: Tko je, Jahve, poput tebe koji ubogog spasavaš od silnika, jadnika i siromaha od pljačkaša?
11 Mashahidi wakatili wanainuka, wananiuliza mambo nisiyoyajua.
Ustadoše svjedoci opaki: pitaju me za ono što ne znam.
12 Wananilipa baya kwa jema na kuiacha nafsi yangu ukiwa.
Vraćaju mi zlo za dobro, duša moja zapada u osamu.
13 Lakini walipokuwa wagonjwa, nilivaa nguo ya gunia na nikajinyenyekesha kwa kufunga. Maombi yangu yaliponirudia bila kujibiwa,
U bolesti njihovoj nosio sam kostrijet, dušu svoju postom morio, i molitva mi se u krilo vraćala.
14 niliendelea kuomboleza kama vile wao ni rafiki au ndugu. Niliinamisha kichwa chini kwa huzuni kama ninayemwombolezea mama yangu.
Kao za prijateljem, za bratom - obilažah tužan; od žalosti se pogurih kao onaj što za majkom žali.
15 Lakini nilipojikwaa, walikusanyika kwa shangwe; washambuliaji walijikusanya dhidi yangu bila mimi kujua. Walinisingizia pasipo kukoma.
A sada kad posrnuh ja, oni se raduju, skupiše se protiv mene da udare iznenada, i bez prestanka oni me razdiru.
16 Kama watu wasiomcha Mungu, wamenidhihaki, wamenisagia meno.
Ruglom na ruglo iskušavaju me i zubima škripaju na mene.
17 Ee Bwana, utatazama mpaka lini? Niokoe maisha yangu na maangamizi yao, uhai wangu wa thamani kutokana na simba hawa.
O Jahve, dokle ćeš gledati? Istrgni mi dušu nasrtajima njihovim, otmi lavovima jedino dobro moje!
18 Nami nitakushukuru mbele ya kusanyiko kubwa, nitakusifu katikati ya watu wengi.
Zahvalit ću ti u velikom zboru, slavit ću te među pukom brojnim.
19 Usiwaache wale wanaonisimanga, wale ambao ni adui zangu bila sababu; usiwaache wale ambao ni adui zangu bila sababu wakonyeze jicho kwa hila.
Nek' se ne raduju nada mnom dušmani nepravedni, nek' ne namiguju očima oni koji me nizašto mrze!
20 Hawazungumzi kwa amani, bali wanatunga mashtaka ya uongo dhidi ya wale wanaoishi kwa utulivu katika nchi.
Jer oni ne misle o miru, već spletke snuju protiv mirnih u zemlji.
21 Hunifumbulia vinywa vyao wakisema, “Aha! Aha! Kwa macho yetu wenyewe tumeliona.”
Razvaljuju svoja usta na me i govore: “Ha, ha, vidjesmo očima svojim!”
22 Ee Bwana, umeona hili, usiwe kimya. Usiwe mbali nami, Ee Bwana.
Ti sve vidiš, o Jahve! Nemoj šutjeti! Gospode, od mene se ne udaljuj!
23 Amka, inuka unitetee! Unipiganie Mungu wangu na Bwana wangu.
Preni se, ustani da me obraniš, Bože moj, Gospode, vodi parnicu moju!
24 Nihukumu kwa haki yako, Ee Bwana Mungu wangu, sawasawa na haki yako; usiwaache wakusimange.
Po svojoj me pravdi sudi, Jahve, Bože moj, nek' se ne raduju nada mnom!
25 Usiwaache wafikiri, “Aha, hili ndilo tulilotaka!” Au waseme, “Tumemmeza.”
Nek' ne misle u srcu: “Ispunila nam se želja!” Nek' ne reknu: “Progutali smo ga!”
26 Wote wanaofurahia dhiki yangu waaibishwe na wachanganyikiwe; hao wanaojiinua dhidi yangu wavikwe aibu na dharau.
Nek' se postide i posrame svi zajedno koji se nesreći mojoj raduju! Nek' se odjenu stidom i sramotom oni koji se podižu na me!
27 Wale wanaofurahia hukumu yangu ya haki wapige kelele za shangwe na furaha; hebu waseme siku zote, “Bwana atukuzwe, ambaye amefurahia mafanikio ya mtumishi wake.”
Nek' radosno kliču kojima je pravo moje na srcu i nek' svagda govore: “Velik je Jahve! Milo mu je spasenje sluge njegova!”
28 Ulimi wangu utanena haki yako na sifa zako mchana kutwa.
A moj će jezik kazivati pravdu tvoju i hvalu tebi navijeke.

< Zaburi 35 >