< Zaburi 34 >

1 Zaburi ya Daudi, alipojifanya mwendawazimu mbele ya Abimeleki, ambaye alimfukuza, naye akaondoka. Nitamtukuza Bwana nyakati zote, sifa zake zitakuwa midomoni mwangu siku zote.
Bendeciré a Yavé en todo tiempo. Su alabanza estará de continuo en mi boca.
2 Nafsi yangu itajisifu katika Bwana, walioonewa watasikia na wafurahi.
En Yavé se gloriará mi alma. Lo oirán los mansos y se alegrarán.
3 Mtukuzeni Bwana pamoja nami, naam, na tulitukuze jina lake pamoja.
Engrandezcan a Yavé conmigo, Y exaltemos juntos su Nombre.
4 Nilimtafuta Bwana naye akanijibu, akaniokoa kwenye hofu zangu zote.
Busqué a Yavé y Él me respondió, Y me libró de todos mis temores.
5 Wale wamtazamao hutiwa nuru, nyuso zao hazifunikwi na aibu kamwe.
Los que miraron a Él fueron iluminados, Y sus semblantes nunca serán avergonzados.
6 Maskini huyu alimwita Bwana, naye akamsikia, akamwokoa katika taabu zake zote.
Este pobre clamó, Y Yavé lo escuchó, Y lo salvó de todas sus angustias.
7 Malaika wa Bwana hufanya kituo akiwazunguka wale wamchao, naye huwaokoa.
El Ángel de Yavé acampa alrededor de los que le temen, Y los rescata.
8 Onjeni mwone kwamba Bwana ni mwema, heri mtu yule anayemkimbilia.
Prueben y vean que Yavé es bueno. ¡Cuán feliz es el varón que confía en Él!
9 Mcheni Bwana enyi watakatifu wake, kwa maana wale wamchao hawapungukiwi na chochote.
Teman a Yavé, ustedes sus santos, Porque nada falta a los que le temen.
10 Wana simba wenye nguvu hutindikiwa na kuona njaa, bali wale wamtafutao Bwana hawatakosa kitu chochote kilicho chema.
Los cachorros de león necesitan y sufren hambre, Pero los que buscan a Yavé no carecen de ningún bien.
11 Njooni, watoto wangu, mnisikilize, nitawafundisha kumcha Bwana.
Vengan, hijos, escúchenme. Les enseñaré el temor a Yavé.
12 Yeyote kati yenu anayependa uzima na kutamani kuziona siku nyingi njema,
¿Quién es el hombre que desea vida, Que desea muchos días para ver el bien?
13 basi auzuie ulimi wake na mabaya, na midomo yake kutokana na kusema uongo.
Guarda tu boca del mal Y tus labios de hablar engaño.
14 Aache uovu, atende mema, aitafute amani na kuifuatilia.
Apártate del mal y haz el bien. Busca la paz y persíguela.
15 Macho ya Bwana huwaelekea wenye haki, na masikio yake yako makini kusikiliza kilio chao.
Los ojos de Yavé están hacia los justos, Y sus oídos atentos al clamor de ellos.
16 Uso wa Bwana uko kinyume na watendao maovu, ili kufuta kumbukumbu lao duniani.
El rostro de Yavé está contra los perversos, Para cortar su memoria de la tierra.
17 Wenye haki hulia, naye Bwana huwasikia, huwaokoa katika taabu zao zote.
Claman los justos, Y Yavé los oye Y los libra de todas sus angustias.
18 Bwana yu karibu na waliovunjika moyo, na huwaokoa waliopondeka roho.
Cercano está Yavé a los quebrantados de corazón, Y salva a los contritos de espíritu.
19 Mwenye haki ana mateso mengi, lakini Bwana humwokoa nayo yote,
Muchas son las aflicciones del justo, Pero de todas ellas lo libra Yavé.
20 huhifadhi mifupa yake yote, hata mmoja hautavunjika.
Él guarda todos sus huesos. Ni uno de ellos es quebrado.
21 Ubaya utamuua mtu mwovu, nao adui za mwenye haki watahukumiwa.
Matará al malo la maldad, Y los que aborrecen al justo serán culpables.
22 Bwana huwakomboa watumishi wake, yeyote anayemkimbilia yeye hatahukumiwa kamwe.
Yavé redime la vida de sus esclavos. No serán condenados cuantos en Él confían.

< Zaburi 34 >