< Zaburi 34 >

1 Zaburi ya Daudi, alipojifanya mwendawazimu mbele ya Abimeleki, ambaye alimfukuza, naye akaondoka. Nitamtukuza Bwana nyakati zote, sifa zake zitakuwa midomoni mwangu siku zote.
Por David; cuando fingió estar loco ante Abimelec, quien lo expulsó, y él se marchó. Bendeciré a Yahvé en todo momento. Su alabanza siempre estará en mi boca.
2 Nafsi yangu itajisifu katika Bwana, walioonewa watasikia na wafurahi.
Mi alma se jactará en Yahvé. Los humildes lo oirán y se alegrarán.
3 Mtukuzeni Bwana pamoja nami, naam, na tulitukuze jina lake pamoja.
Oh, engrandece a Yahvé conmigo. Exaltemos juntos su nombre.
4 Nilimtafuta Bwana naye akanijibu, akaniokoa kwenye hofu zangu zote.
Busqué a Yahvé y me respondió, y me libró de todos mis temores.
5 Wale wamtazamao hutiwa nuru, nyuso zao hazifunikwi na aibu kamwe.
Lo miraron y quedaron radiantes. Sus rostros nunca se cubrirán de vergüenza.
6 Maskini huyu alimwita Bwana, naye akamsikia, akamwokoa katika taabu zake zote.
Este pobre hombre clamó, y Yahvé lo escuchó, y lo salvó de todos sus problemas.
7 Malaika wa Bwana hufanya kituo akiwazunguka wale wamchao, naye huwaokoa.
El ángel de Yahvé acampa alrededor de los que le temen, y los entrega.
8 Onjeni mwone kwamba Bwana ni mwema, heri mtu yule anayemkimbilia.
Oh, probad y ved que Yahvé es bueno. Dichoso el hombre que se refugia en él.
9 Mcheni Bwana enyi watakatifu wake, kwa maana wale wamchao hawapungukiwi na chochote.
Temed a Yahvé, vosotros sus santos, porque no hay falta con los que le temen.
10 Wana simba wenye nguvu hutindikiwa na kuona njaa, bali wale wamtafutao Bwana hawatakosa kitu chochote kilicho chema.
Los leones jóvenes carecen y sufren hambre, pero a los que buscan a Yahvé no les faltará nada bueno.
11 Njooni, watoto wangu, mnisikilize, nitawafundisha kumcha Bwana.
Venid, niños, escuchadme. Te enseñaré el temor de Yahvé.
12 Yeyote kati yenu anayependa uzima na kutamani kuziona siku nyingi njema,
Que es alguien que desea la vida, y ama muchos días, para que vea el bien?
13 basi auzuie ulimi wake na mabaya, na midomo yake kutokana na kusema uongo.
Guarda tu lengua del mal, y tus labios de decir mentiras.
14 Aache uovu, atende mema, aitafute amani na kuifuatilia.
Apártate del mal y haz el bien. Busca la paz y persíguela.
15 Macho ya Bwana huwaelekea wenye haki, na masikio yake yako makini kusikiliza kilio chao.
Los ojos de Yahvé están hacia los justos. Sus oídos escuchan su grito.
16 Uso wa Bwana uko kinyume na watendao maovu, ili kufuta kumbukumbu lao duniani.
El rostro de Yahvé está contra los que hacen el mal, para cortar su memoria de la tierra.
17 Wenye haki hulia, naye Bwana huwasikia, huwaokoa katika taabu zao zote.
Los justos claman, y Yahvé los escucha, y los libra de todos sus problemas.
18 Bwana yu karibu na waliovunjika moyo, na huwaokoa waliopondeka roho.
Yahvé está cerca de los que tienen el corazón roto, y salva a los que tienen el espíritu abatido.
19 Mwenye haki ana mateso mengi, lakini Bwana humwokoa nayo yote,
Muchas son las aflicciones de los justos, pero Yahvé lo libra de todos ellos.
20 huhifadhi mifupa yake yote, hata mmoja hautavunjika.
Protege todos sus huesos. Ninguno de ellos está roto.
21 Ubaya utamuua mtu mwovu, nao adui za mwenye haki watahukumiwa.
El mal matará a los malvados. Los que odian a los justos serán condenados.
22 Bwana huwakomboa watumishi wake, yeyote anayemkimbilia yeye hatahukumiwa kamwe.
Yahvé redimeel alma de sus siervos. Ninguno de los que se refugian en él será condenado.

< Zaburi 34 >