< Zaburi 34 >
1 Zaburi ya Daudi, alipojifanya mwendawazimu mbele ya Abimeleki, ambaye alimfukuza, naye akaondoka. Nitamtukuza Bwana nyakati zote, sifa zake zitakuwa midomoni mwangu siku zote.
Псалом Давиду, внегда измени лице свое пред Авимелехом: и отпусти его, и отиде. Благословлю Господа на всякое время, выну хвала Его во устех моих.
2 Nafsi yangu itajisifu katika Bwana, walioonewa watasikia na wafurahi.
О Господе похвалится душа моя: да услышат кротцыи и возвеселятся.
3 Mtukuzeni Bwana pamoja nami, naam, na tulitukuze jina lake pamoja.
Возвеличите Господа со мною, и вознесем имя Его вкупе.
4 Nilimtafuta Bwana naye akanijibu, akaniokoa kwenye hofu zangu zote.
Взысках Господа, и услыша мя и от всех скорбей моих избави мя.
5 Wale wamtazamao hutiwa nuru, nyuso zao hazifunikwi na aibu kamwe.
Приступите к Нему и просветитеся, и лица ваша не постыдятся.
6 Maskini huyu alimwita Bwana, naye akamsikia, akamwokoa katika taabu zake zote.
Сей нищий воззва, и Господь услыша и, и от всех скорбей его спасе и.
7 Malaika wa Bwana hufanya kituo akiwazunguka wale wamchao, naye huwaokoa.
Ополчится Ангел Господень окрест боящихся Его и избавит их.
8 Onjeni mwone kwamba Bwana ni mwema, heri mtu yule anayemkimbilia.
Вкусите и видите, яко благ Господь: блажен муж, иже уповает Нань.
9 Mcheni Bwana enyi watakatifu wake, kwa maana wale wamchao hawapungukiwi na chochote.
Бойтеся Господа, вси святии Его, яко несть лишения боящымся Его.
10 Wana simba wenye nguvu hutindikiwa na kuona njaa, bali wale wamtafutao Bwana hawatakosa kitu chochote kilicho chema.
Богатии обнищаша и взалкаша: взыскающии же Господа не лишатся всякаго блага.
11 Njooni, watoto wangu, mnisikilize, nitawafundisha kumcha Bwana.
Приидите, чада, послушайте мене, страху Господню научу вас.
12 Yeyote kati yenu anayependa uzima na kutamani kuziona siku nyingi njema,
Кто есть человек хотяй живот, любяй дни видети благи?
13 basi auzuie ulimi wake na mabaya, na midomo yake kutokana na kusema uongo.
Удержи язык твой от зла и устне твои, еже не глаголати льсти.
14 Aache uovu, atende mema, aitafute amani na kuifuatilia.
Уклонися от зла и сотвори благо: взыщи мира и пожени и.
15 Macho ya Bwana huwaelekea wenye haki, na masikio yake yako makini kusikiliza kilio chao.
Очи Господни на праведныя, и уши Его в молитву их.
16 Uso wa Bwana uko kinyume na watendao maovu, ili kufuta kumbukumbu lao duniani.
Лице же Господне на творящыя злая, еже потребити от земли память их.
17 Wenye haki hulia, naye Bwana huwasikia, huwaokoa katika taabu zao zote.
Воззваша праведнии, и Господь услыша их и от всех скорбей их избави их.
18 Bwana yu karibu na waliovunjika moyo, na huwaokoa waliopondeka roho.
Близ Господь сокрушенных сердцем, и смиренныя духом спасет.
19 Mwenye haki ana mateso mengi, lakini Bwana humwokoa nayo yote,
Многи скорби праведным, и от всех их избавит я Господь.
20 huhifadhi mifupa yake yote, hata mmoja hautavunjika.
Хранит Господь вся кости их, ни едина от них сокрушится.
21 Ubaya utamuua mtu mwovu, nao adui za mwenye haki watahukumiwa.
Смерть грешников люта, и ненавидящии праведнаго прегрешат.
22 Bwana huwakomboa watumishi wake, yeyote anayemkimbilia yeye hatahukumiwa kamwe.
Избавит Господь душы раб Своих, и не прегрешат вси уповающии на Него.