< Zaburi 34 >

1 Zaburi ya Daudi, alipojifanya mwendawazimu mbele ya Abimeleki, ambaye alimfukuza, naye akaondoka. Nitamtukuza Bwana nyakati zote, sifa zake zitakuwa midomoni mwangu siku zote.
[Salmo] di Davide, intorno a ciò ch'egli si contraffece davanti ad Abimelec; onde esso lo cacciò via, ed egli se ne andò IO benedirò il Signore in ogni tempo; La sua lode [sarà] sempre nella mia bocca.
2 Nafsi yangu itajisifu katika Bwana, walioonewa watasikia na wafurahi.
L'anima mia si glorierà nel Signore; Gli umili l'udiranno, e si rallegreranno.
3 Mtukuzeni Bwana pamoja nami, naam, na tulitukuze jina lake pamoja.
Magnificate meco il Signore, Ed esaltiamo [tutti] insieme il suo Nome.
4 Nilimtafuta Bwana naye akanijibu, akaniokoa kwenye hofu zangu zote.
Io ho cercato il Signore, ed egli mi ha risposto, E mi ha liberato da tutti i miei spaventi.
5 Wale wamtazamao hutiwa nuru, nyuso zao hazifunikwi na aibu kamwe.
Quelli che hanno riguardato a lui sono stati illuminati, E le lor facce non sono state svergognate.
6 Maskini huyu alimwita Bwana, naye akamsikia, akamwokoa katika taabu zake zote.
Questo povero afflitto ha gridato, e il Signore l'ha esaudito, E l'ha salvato da tutte le sue distrette.
7 Malaika wa Bwana hufanya kituo akiwazunguka wale wamchao, naye huwaokoa.
Gli Angeli del Signore sono accampati intorno a quelli che lo temono, E li liberano.
8 Onjeni mwone kwamba Bwana ni mwema, heri mtu yule anayemkimbilia.
Gustate, e vedete quanto il Signore [è] buono; Beato l'uomo [che] spera in lui.
9 Mcheni Bwana enyi watakatifu wake, kwa maana wale wamchao hawapungukiwi na chochote.
Temete il Signore, [voi] suoi santi; Poichè nulla manca a quelli che lo temono.
10 Wana simba wenye nguvu hutindikiwa na kuona njaa, bali wale wamtafutao Bwana hawatakosa kitu chochote kilicho chema.
I leoncelli soffrono necessità e fame; Ma quelli che cercano il Signore non hanno mancamento di alcun bene.
11 Njooni, watoto wangu, mnisikilize, nitawafundisha kumcha Bwana.
Venite, figliuoli, ascoltatemi; Io v'insegnerò il timor del Signore.
12 Yeyote kati yenu anayependa uzima na kutamani kuziona siku nyingi njema,
Quale [è] l'uomo che abbia voglia di vivere, Che ami [lunghezza di] giorni per veder del bene?
13 basi auzuie ulimi wake na mabaya, na midomo yake kutokana na kusema uongo.
Guarda la tua lingua dal male, E le tue labbra da parlar frode.
14 Aache uovu, atende mema, aitafute amani na kuifuatilia.
Ritratti dal male, e fa' il bene; Cerca la pace, e procacciala.
15 Macho ya Bwana huwaelekea wenye haki, na masikio yake yako makini kusikiliza kilio chao.
Gli occhi del Signore [son] verso i giusti, E le sue orecchie [sono attente] al grido loro.
16 Uso wa Bwana uko kinyume na watendao maovu, ili kufuta kumbukumbu lao duniani.
La faccia del Signore [è] contro a quelli che fanno male, Per isterminare la lor memoria d'in su la terra.
17 Wenye haki hulia, naye Bwana huwasikia, huwaokoa katika taabu zao zote.
[I giusti] gridano, e il Signore [li] esaudisce, E li libera da tutte le lor distrette.
18 Bwana yu karibu na waliovunjika moyo, na huwaokoa waliopondeka roho.
Il Signore [è] presso di quelli che hanno il cuor rotto, E salva quelli che hanno lo spirito contrito.
19 Mwenye haki ana mateso mengi, lakini Bwana humwokoa nayo yote,
Molte [son] le afflizioni del giusto; Ma il Signore lo libererà da tutte.
20 huhifadhi mifupa yake yote, hata mmoja hautavunjika.
Egli guarda tutte le ossa di esso: E niuno ne può esser rotto.
21 Ubaya utamuua mtu mwovu, nao adui za mwenye haki watahukumiwa.
La malvagità farà morire il malvagio, E quelli che odiano il giusto saran distrutti.
22 Bwana huwakomboa watumishi wake, yeyote anayemkimbilia yeye hatahukumiwa kamwe.
Il Signore riscatta l'anima de' suoi servitori; E niuno di quelli che sperano in lui sarà distrutto.

< Zaburi 34 >