< Zaburi 34 >

1 Zaburi ya Daudi, alipojifanya mwendawazimu mbele ya Abimeleki, ambaye alimfukuza, naye akaondoka. Nitamtukuza Bwana nyakati zote, sifa zake zitakuwa midomoni mwangu siku zote.
Psaume par David, lorsqu’il changea son visage devant Achimélech, qui le renvoya, et qu’il s’en alla. Je bénirai le Seigneur en tout temps: toujours sa louange sera dans ma bouche.
2 Nafsi yangu itajisifu katika Bwana, walioonewa watasikia na wafurahi.
Mon âme se glorifiera dans le Seigneur: que les hommes doux m’entendent et qu’ils soient comblés de joie.
3 Mtukuzeni Bwana pamoja nami, naam, na tulitukuze jina lake pamoja.
Glorifiez le Seigneur avec moi: et exaltons tous pareillement son nom.
4 Nilimtafuta Bwana naye akanijibu, akaniokoa kwenye hofu zangu zote.
J’ai recherché le Seigneur, et il m’a exaucé, et il m’a retiré de toutes mes tribulations.
5 Wale wamtazamao hutiwa nuru, nyuso zao hazifunikwi na aibu kamwe.
Approchez de lui, et vous serez éclairés, et vos faces n’éprouveront pas la confusion.
6 Maskini huyu alimwita Bwana, naye akamsikia, akamwokoa katika taabu zake zote.
Ce pauvre a crié, et le Seigneur l’a exaucé, et il l’a sauvé de toutes ses tribulations.
7 Malaika wa Bwana hufanya kituo akiwazunguka wale wamchao, naye huwaokoa.
Un ange du Seigneur se placera autour de ceux qui le craignent, et il les délivrera.
8 Onjeni mwone kwamba Bwana ni mwema, heri mtu yule anayemkimbilia.
Goûtez et voyez combien le Seigneur est doux: heureux l’homme qui espère en lui.
9 Mcheni Bwana enyi watakatifu wake, kwa maana wale wamchao hawapungukiwi na chochote.
Craignez le Seigneur, vous tous ses saints, parce qu’il n’y a pas d’indigence pour ceux qui le craignent.
10 Wana simba wenye nguvu hutindikiwa na kuona njaa, bali wale wamtafutao Bwana hawatakosa kitu chochote kilicho chema.
Des riches ont été dans le besoin, et ont eu faim; mais ceux qui cherchent le Seigneur n’éprouveront l’amoindrissement d’aucun bien.
11 Njooni, watoto wangu, mnisikilize, nitawafundisha kumcha Bwana.
Venez, mes enfants, écoutez-moi: je vous enseignerai la crainte du Seigneur.
12 Yeyote kati yenu anayependa uzima na kutamani kuziona siku nyingi njema,
Quel est l’homme qui veut une vie heureuse, qui aime à voir des jours de bonheur?
13 basi auzuie ulimi wake na mabaya, na midomo yake kutokana na kusema uongo.
Préserve ta langue du mal; et que tes lèvres ne profèrent point de discours artificieux.
14 Aache uovu, atende mema, aitafute amani na kuifuatilia.
Détourne-toi du mal et fais le bien; cherche la paix, poursuis-la.
15 Macho ya Bwana huwaelekea wenye haki, na masikio yake yako makini kusikiliza kilio chao.
Les yeux du Seigneur sont sur les justes, et ses oreilles à leurs prières.
16 Uso wa Bwana uko kinyume na watendao maovu, ili kufuta kumbukumbu lao duniani.
Mais le visage du Seigneur est sur ceux qui font le mal, afin d’effacer de la terre leur mémoire.
17 Wenye haki hulia, naye Bwana huwasikia, huwaokoa katika taabu zao zote.
Les justes ont crié, et le Seigneur les a exaucés: et il les a délivrés de toutes leurs tribulations.
18 Bwana yu karibu na waliovunjika moyo, na huwaokoa waliopondeka roho.
Le Seigneur est près de ceux qui ont le cœur affligé; et il sauvera les humbles d’esprit.
19 Mwenye haki ana mateso mengi, lakini Bwana humwokoa nayo yote,
Nombreuses sont les tribulations des Justes; mais Dieu les délivrera de toutes ces peines.
20 huhifadhi mifupa yake yote, hata mmoja hautavunjika.
Le Seigneur garde tous leurs os: et pas un seul ne sera brisé.
21 Ubaya utamuua mtu mwovu, nao adui za mwenye haki watahukumiwa.
La mort des pécheurs est très funeste; et ceux qui haïssent le juste seront traités comme coupables.
22 Bwana huwakomboa watumishi wake, yeyote anayemkimbilia yeye hatahukumiwa kamwe.
Le Seigneur rachètera l’âme de ses serviteurs: et nul de ceux qui espèrent en lui ne sera traité comme coupable.

< Zaburi 34 >