< Zaburi 34 >

1 Zaburi ya Daudi, alipojifanya mwendawazimu mbele ya Abimeleki, ambaye alimfukuza, naye akaondoka. Nitamtukuza Bwana nyakati zote, sifa zake zitakuwa midomoni mwangu siku zote.
Psaume de David, quand il changea de contenance devant Abimélech, qui le laissa partir, et il partit. En tout temps je bénirai le Seigneur; sa louange sera en tout temps dans ma bouche.
2 Nafsi yangu itajisifu katika Bwana, walioonewa watasikia na wafurahi.
Mon âme se réjouira dans le Seigneur; que les doux écoutent et se réjouissent.
3 Mtukuzeni Bwana pamoja nami, naam, na tulitukuze jina lake pamoja.
Glorifiez avec moi le Seigneur, et exaltons son nom tous ensemble.
4 Nilimtafuta Bwana naye akanijibu, akaniokoa kwenye hofu zangu zote.
J'ai cherché le Seigneur, et il m'a exaucé; il m'a tiré de toutes mes afflictions.
5 Wale wamtazamao hutiwa nuru, nyuso zao hazifunikwi na aibu kamwe.
Approchez-vous de lui, éclairez-vous de sa lumière, et vos faces ne seront point confondues.
6 Maskini huyu alimwita Bwana, naye akamsikia, akamwokoa katika taabu zake zote.
Le pauvre a crié et le Seigneur l'a exaucé, et il l'a délivré de toutes ses afflictions.
7 Malaika wa Bwana hufanya kituo akiwazunguka wale wamchao, naye huwaokoa.
L'ange du Seigneur veillera autour de ceux qui craignent Dieu, et il les sauvera.
8 Onjeni mwone kwamba Bwana ni mwema, heri mtu yule anayemkimbilia.
Goûtez et voyez combien le Seigneur est doux; heureux l'homme qui espère en lui.
9 Mcheni Bwana enyi watakatifu wake, kwa maana wale wamchao hawapungukiwi na chochote.
Craignez le Seigneur, vous tous qui êtes ses saints; car rien ne manque à ceux qui le craignent.
10 Wana simba wenye nguvu hutindikiwa na kuona njaa, bali wale wamtafutao Bwana hawatakosa kitu chochote kilicho chema.
Les riches sont devenus pauvres et ils ont eu faim; mais ceux qui cherchent le Seigneur ne manqueront d'aucun bien. Interlude.
11 Njooni, watoto wangu, mnisikilize, nitawafundisha kumcha Bwana.
Venez, enfants, écoutez-moi; je vous enseignerai la crainte du Seigneur.
12 Yeyote kati yenu anayependa uzima na kutamani kuziona siku nyingi njema,
Quel est l'homme qui veut la vie, qui désire voir des jours heureux?
13 basi auzuie ulimi wake na mabaya, na midomo yake kutokana na kusema uongo.
Que sa langue s'abstienne du mal, et ses lèvres du mensonge.
14 Aache uovu, atende mema, aitafute amani na kuifuatilia.
Détourne-toi du mal, et fais le bien; cherche la paix et la poursuis.
15 Macho ya Bwana huwaelekea wenye haki, na masikio yake yako makini kusikiliza kilio chao.
Les yeux du Seigneur sont sur les justes, et ses oreilles vers leurs prières.
16 Uso wa Bwana uko kinyume na watendao maovu, ili kufuta kumbukumbu lao duniani.
Le visage du Seigneur est tourné contre ceux qui font le mal, pour effacer de la terre leur souvenir.
17 Wenye haki hulia, naye Bwana huwasikia, huwaokoa katika taabu zao zote.
Les justes ont crié, et le Seigneur les a exaucés; et il les a délivrés de toutes leurs afflictions.
18 Bwana yu karibu na waliovunjika moyo, na huwaokoa waliopondeka roho.
Le Seigneur est près de ceux dont le cœur est affligé; il sauvera les humbles d'esprit.
19 Mwenye haki ana mateso mengi, lakini Bwana humwokoa nayo yote,
Les afflictions du juste sont nombreuses, et de toutes le Seigneur le délivrera.
20 huhifadhi mifupa yake yote, hata mmoja hautavunjika.
Le Seigneur garde tous leurs os, pas un seul ne sera broyé.
21 Ubaya utamuua mtu mwovu, nao adui za mwenye haki watahukumiwa.
La mort des pécheurs est leur grand malheur, et ceux qui haïssent le juste périront.
22 Bwana huwakomboa watumishi wake, yeyote anayemkimbilia yeye hatahukumiwa kamwe.
Le Seigneur affranchira les âmes de ceux qui le servent, et ceux qui espèrent en lui ne défailliront pas.

< Zaburi 34 >