< Zaburi 34 >

1 Zaburi ya Daudi, alipojifanya mwendawazimu mbele ya Abimeleki, ambaye alimfukuza, naye akaondoka. Nitamtukuza Bwana nyakati zote, sifa zake zitakuwa midomoni mwangu siku zote.
To Dauid, whanne he chaungide his mouth bifor Abymalech, and he `droof out Dauid, `and he yede forth. I schal blesse the Lord in al tyme; euere his heriyng is in my mouth.
2 Nafsi yangu itajisifu katika Bwana, walioonewa watasikia na wafurahi.
Mi soule schal be preisid in the Lord; mylde men here, and be glad.
3 Mtukuzeni Bwana pamoja nami, naam, na tulitukuze jina lake pamoja.
Magnyfie ye the Lord with me; and enhaunse we his name into it silf.
4 Nilimtafuta Bwana naye akanijibu, akaniokoa kwenye hofu zangu zote.
I souyte the Lord, and he herde me; and he delyueride me fro alle my tribulaciouns.
5 Wale wamtazamao hutiwa nuru, nyuso zao hazifunikwi na aibu kamwe.
Neiye ye to him, and be ye liytned; and youre faces schulen not be schent.
6 Maskini huyu alimwita Bwana, naye akamsikia, akamwokoa katika taabu zake zote.
This pore man criede, and the Lord herde hym; and sauyde hym fro alle hise tribulaciouns.
7 Malaika wa Bwana hufanya kituo akiwazunguka wale wamchao, naye huwaokoa.
The aungel of the Lord sendith in the cumpas of men dredynge hym; and he schal delyuere hem.
8 Onjeni mwone kwamba Bwana ni mwema, heri mtu yule anayemkimbilia.
Taaste ye, and se, for the Lord is swete; blessid is the man, that hopith in hym.
9 Mcheni Bwana enyi watakatifu wake, kwa maana wale wamchao hawapungukiwi na chochote.
Alle ye hooli men of the Lord, drede hym; for no nedynesse is to men dredynge hym.
10 Wana simba wenye nguvu hutindikiwa na kuona njaa, bali wale wamtafutao Bwana hawatakosa kitu chochote kilicho chema.
Riche men weren nedi, and weren hungri; but men that seken the Lord schulen not faile of al good.
11 Njooni, watoto wangu, mnisikilize, nitawafundisha kumcha Bwana.
Come, ye sones, here ye me; Y schal teche you the drede of the Lord.
12 Yeyote kati yenu anayependa uzima na kutamani kuziona siku nyingi njema,
Who is a man, that wole lijf; loueth to se good daies?
13 basi auzuie ulimi wake na mabaya, na midomo yake kutokana na kusema uongo.
Forbede thi tunge fro yuel; and thi lippis speke not gile.
14 Aache uovu, atende mema, aitafute amani na kuifuatilia.
Turne thou awei fro yuel, and do good; seke thou pees, and perfitli sue thou it.
15 Macho ya Bwana huwaelekea wenye haki, na masikio yake yako makini kusikiliza kilio chao.
The iyen of the Lord ben on iust men; and hise eeren ben to her preiers.
16 Uso wa Bwana uko kinyume na watendao maovu, ili kufuta kumbukumbu lao duniani.
But the cheer of the Lord is on men doynge yuels; that he leese the mynde of hem fro erthe.
17 Wenye haki hulia, naye Bwana huwasikia, huwaokoa katika taabu zao zote.
Just men cryeden, and the Lord herde hem; and delyueride hem fro alle her tribulaciouns.
18 Bwana yu karibu na waliovunjika moyo, na huwaokoa waliopondeka roho.
The Lord is nyy hem that ben of troblid herte; and he schal saue meke men in spirit.
19 Mwenye haki ana mateso mengi, lakini Bwana humwokoa nayo yote,
Many tribulaciouns ben of iust men; and the Lord schal delyuere hem fro alle these.
20 huhifadhi mifupa yake yote, hata mmoja hautavunjika.
The Lord kepith alle the boonys of hem; oon of tho schal not be brokun.
21 Ubaya utamuua mtu mwovu, nao adui za mwenye haki watahukumiwa.
The deth of synneris is werst; and thei that haten a iust man schulen trespasse.
22 Bwana huwakomboa watumishi wake, yeyote anayemkimbilia yeye hatahukumiwa kamwe.
The Lord schal ayenbie the soulis of hise seruauntis; and alle, that hopen in him, schulen not trespasse.

< Zaburi 34 >