< Zaburi 34 >
1 Zaburi ya Daudi, alipojifanya mwendawazimu mbele ya Abimeleki, ambaye alimfukuza, naye akaondoka. Nitamtukuza Bwana nyakati zote, sifa zake zitakuwa midomoni mwangu siku zote.
Of David, when he feigned madness in the presence of Abimelech, who drove him away, and he left. I will bless the Lord at all times, in my mouth will his praise be forever.
2 Nafsi yangu itajisifu katika Bwana, walioonewa watasikia na wafurahi.
In the Lord will my heart make her boast, the humble will hear and be glad.
3 Mtukuzeni Bwana pamoja nami, naam, na tulitukuze jina lake pamoja.
O magnify the Lord with me and let us extol his name together.
4 Nilimtafuta Bwana naye akanijibu, akaniokoa kwenye hofu zangu zote.
I sought the Lord, and, in answer, he saved me from all my terrors.
5 Wale wamtazamao hutiwa nuru, nyuso zao hazifunikwi na aibu kamwe.
Look to him and you will be radiant, with faces unashamed.
6 Maskini huyu alimwita Bwana, naye akamsikia, akamwokoa katika taabu zake zote.
Here is one who was crushed, but cried and was heard by the Lord, and brought safe out of every trouble.
7 Malaika wa Bwana hufanya kituo akiwazunguka wale wamchao, naye huwaokoa.
The Lord’s angel encamps about those who fear him, and rescues them.
8 Onjeni mwone kwamba Bwana ni mwema, heri mtu yule anayemkimbilia.
O taste and see that the Lord is good, happy those who take refuge in him.
9 Mcheni Bwana enyi watakatifu wake, kwa maana wale wamchao hawapungukiwi na chochote.
Fear the Lord, all his people, for they who fear him lack nothing.
10 Wana simba wenye nguvu hutindikiwa na kuona njaa, bali wale wamtafutao Bwana hawatakosa kitu chochote kilicho chema.
Even young lions may be poor and hungry, but those who seek the Lord will not lack any good thing.
11 Njooni, watoto wangu, mnisikilize, nitawafundisha kumcha Bwana.
Come, children, listen to me. I will teach you the fear of the Lord.
12 Yeyote kati yenu anayependa uzima na kutamani kuziona siku nyingi njema,
Which of you is desirous of life, loves many and happy days?
13 basi auzuie ulimi wake na mabaya, na midomo yake kutokana na kusema uongo.
Then guard your tongue from evil, and your lips from speaking deceit.
14 Aache uovu, atende mema, aitafute amani na kuifuatilia.
Depart from evil, and do good; seek peace, and pursue it.
15 Macho ya Bwana huwaelekea wenye haki, na masikio yake yako makini kusikiliza kilio chao.
The eyes of the Lord are towards the righteous, his ears are towards their cry for help.
16 Uso wa Bwana uko kinyume na watendao maovu, ili kufuta kumbukumbu lao duniani.
The Lord sets his face against those who do evil, to root their memory out of the earth.
17 Wenye haki hulia, naye Bwana huwasikia, huwaokoa katika taabu zao zote.
When righteous cry, they are heard by the Lord, and he saves them from all their distresses.
18 Bwana yu karibu na waliovunjika moyo, na huwaokoa waliopondeka roho.
The Lord is near to the broken-hearted, he helps those whose spirit is crushed.
19 Mwenye haki ana mateso mengi, lakini Bwana humwokoa nayo yote,
Many misfortunes befall the righteous, but the Lord delivers them out of them all.
20 huhifadhi mifupa yake yote, hata mmoja hautavunjika.
He guards all their bones, none are broken.
21 Ubaya utamuua mtu mwovu, nao adui za mwenye haki watahukumiwa.
Misfortune will slay the ungodly; those who hate the righteous are doomed.
22 Bwana huwakomboa watumishi wake, yeyote anayemkimbilia yeye hatahukumiwa kamwe.
The Lord ransoms the life of his servants, and none will be doomed who takes refuge in him.