< Zaburi 34 >
1 Zaburi ya Daudi, alipojifanya mwendawazimu mbele ya Abimeleki, ambaye alimfukuza, naye akaondoka. Nitamtukuza Bwana nyakati zote, sifa zake zitakuwa midomoni mwangu siku zote.
א I will bless Adonai at all times. His tehilah ·praise song· will always be in my mouth.
2 Nafsi yangu itajisifu katika Bwana, walioonewa watasikia na wafurahi.
בּ My soul shall boast in Adonai. The humble shall sh'ma ·hear obey· it, and be glad.
3 Mtukuzeni Bwana pamoja nami, naam, na tulitukuze jina lake pamoja.
גּ Oh magnify Adonai with me. Let us exalt his name together.
4 Nilimtafuta Bwana naye akanijibu, akaniokoa kwenye hofu zangu zote.
דּ I sought Adonai, and he answered me, and delivered me from all my fears.
5 Wale wamtazamao hutiwa nuru, nyuso zao hazifunikwi na aibu kamwe.
ה They looked to him, and were radiant. Their faces shall never be covered with shame.
6 Maskini huyu alimwita Bwana, naye akamsikia, akamwokoa katika taabu zake zote.
ז This poor man cried, and Adonai sh'ma ·heard obeyed· him, and saved him out of all his troubles.
7 Malaika wa Bwana hufanya kituo akiwazunguka wale wamchao, naye huwaokoa.
ח Ha mal'ak Yahweh [The Angel of He sustains breathing] encamps around those who fear him, and delivers them.
8 Onjeni mwone kwamba Bwana ni mwema, heri mtu yule anayemkimbilia.
ט Oh taste and see that Adonai is good. Blessed is the man who takes refuge in him.
9 Mcheni Bwana enyi watakatifu wake, kwa maana wale wamchao hawapungukiwi na chochote.
י Oh fear Adonai, you his saints, for there is no lack with those who fear him.
10 Wana simba wenye nguvu hutindikiwa na kuona njaa, bali wale wamtafutao Bwana hawatakosa kitu chochote kilicho chema.
כּ The young lions do lack, and suffer hunger, but those who seek Adonai shall not lack any good thing.
11 Njooni, watoto wangu, mnisikilize, nitawafundisha kumcha Bwana.
ל Come, you children, sh'ma ·hear obey· unto me. I will teach you the fear of Adonai.
12 Yeyote kati yenu anayependa uzima na kutamani kuziona siku nyingi njema,
מ Who of you takes pleasure in living? Who 'ahav ·affectionately loves· a long life to see good things?
13 basi auzuie ulimi wake na mabaya, na midomo yake kutokana na kusema uongo.
נ [If you do], keep your tongue from evil, and your lips from deceiving talk;
14 Aache uovu, atende mema, aitafute amani na kuifuatilia.
ס turn from evil, and do good. Seek peace, and fervently pursue it!
15 Macho ya Bwana huwaelekea wenye haki, na masikio yake yako makini kusikiliza kilio chao.
ע For Adonai’s eyes are toward the upright. His ears listen to their prayers.
16 Uso wa Bwana uko kinyume na watendao maovu, ili kufuta kumbukumbu lao duniani.
פּ But Adonai’s face is against those who do evil, to cut off their memory from the earth.
17 Wenye haki hulia, naye Bwana huwasikia, huwaokoa katika taabu zao zote.
צ The upright cry, and Adonai sh'ma ·hears obeys·, and delivers them out of all their troubles.
18 Bwana yu karibu na waliovunjika moyo, na huwaokoa waliopondeka roho.
ק Adonai is near to those who have a broken heart, and saves those who have a crushed spirit.
19 Mwenye haki ana mateso mengi, lakini Bwana humwokoa nayo yote,
ר Many are the afflictions of the righteous, but Adonai delivers him out of them all.
20 huhifadhi mifupa yake yote, hata mmoja hautavunjika.
שׁ He protects all of his bones. Not one of them is broken.
21 Ubaya utamuua mtu mwovu, nao adui za mwenye haki watahukumiwa.
תּ Evil shall kill the wicked. Those who hate the upright shall be condemned guilty.
22 Bwana huwakomboa watumishi wake, yeyote anayemkimbilia yeye hatahukumiwa kamwe.
Adonai redeems the soul of his servants. None of those who take refuge in him shall be condemned guilty.