< Zaburi 34 >

1 Zaburi ya Daudi, alipojifanya mwendawazimu mbele ya Abimeleki, ambaye alimfukuza, naye akaondoka. Nitamtukuza Bwana nyakati zote, sifa zake zitakuwa midomoni mwangu siku zote.
To David, when he changed his appearance in the sight of Abimelech, and so he dismissed him, and he went away. I will bless the Lord at all times. His praise will be ever in my mouth.
2 Nafsi yangu itajisifu katika Bwana, walioonewa watasikia na wafurahi.
In the Lord, my soul will be praised. May the meek listen and rejoice.
3 Mtukuzeni Bwana pamoja nami, naam, na tulitukuze jina lake pamoja.
Magnify the Lord with me, and let us extol his name in itself.
4 Nilimtafuta Bwana naye akanijibu, akaniokoa kwenye hofu zangu zote.
I sought the Lord, and he heeded me, and he carried me away from all my tribulations.
5 Wale wamtazamao hutiwa nuru, nyuso zao hazifunikwi na aibu kamwe.
Approach him and be enlightened, and your faces will not be confounded.
6 Maskini huyu alimwita Bwana, naye akamsikia, akamwokoa katika taabu zake zote.
This poor one cried out, and the Lord heeded him, and he saved him from all his tribulations.
7 Malaika wa Bwana hufanya kituo akiwazunguka wale wamchao, naye huwaokoa.
The Angel of the Lord will encamp around those who fear him, and he will rescue them.
8 Onjeni mwone kwamba Bwana ni mwema, heri mtu yule anayemkimbilia.
Taste and see that the Lord is sweet. Blessed is the man who hopes in him.
9 Mcheni Bwana enyi watakatifu wake, kwa maana wale wamchao hawapungukiwi na chochote.
Fear the Lord, all you his saints. For there is no destitution for those who fear him.
10 Wana simba wenye nguvu hutindikiwa na kuona njaa, bali wale wamtafutao Bwana hawatakosa kitu chochote kilicho chema.
The rich have been needy and hungry, but those who seek the Lord will not be deprived of any good thing.
11 Njooni, watoto wangu, mnisikilize, nitawafundisha kumcha Bwana.
Come forward, sons. Listen to me. I will teach you the fear of the Lord.
12 Yeyote kati yenu anayependa uzima na kutamani kuziona siku nyingi njema,
Which is the man who wills life, who chooses to see good days?
13 basi auzuie ulimi wake na mabaya, na midomo yake kutokana na kusema uongo.
Prohibit your tongue from evil and your lips from speaking deceit.
14 Aache uovu, atende mema, aitafute amani na kuifuatilia.
Turn away from evil, and do good. Inquire about peace, and pursue it.
15 Macho ya Bwana huwaelekea wenye haki, na masikio yake yako makini kusikiliza kilio chao.
The eyes of the Lord are on the just, and his ears are with their prayers.
16 Uso wa Bwana uko kinyume na watendao maovu, ili kufuta kumbukumbu lao duniani.
But the countenance of the Lord is upon those who do evil, to perish the remembrance of them from the earth.
17 Wenye haki hulia, naye Bwana huwasikia, huwaokoa katika taabu zao zote.
The just cried out, and the Lord heard them, and he freed them from all their tribulations.
18 Bwana yu karibu na waliovunjika moyo, na huwaokoa waliopondeka roho.
The Lord is near to those who are troubled in heart, and he will save the humble in spirit.
19 Mwenye haki ana mateso mengi, lakini Bwana humwokoa nayo yote,
Many are the afflictions of the just, but from them all the Lord will free them.
20 huhifadhi mifupa yake yote, hata mmoja hautavunjika.
The Lord preserves all of their bones, not one of them shall be broken.
21 Ubaya utamuua mtu mwovu, nao adui za mwenye haki watahukumiwa.
The death of a sinner is very harmful, and those who hate the just will fare badly.
22 Bwana huwakomboa watumishi wake, yeyote anayemkimbilia yeye hatahukumiwa kamwe.
The Lord will redeem the souls of his servants, and none of those who hope in him will fare badly.

< Zaburi 34 >