< Zaburi 34 >

1 Zaburi ya Daudi, alipojifanya mwendawazimu mbele ya Abimeleki, ambaye alimfukuza, naye akaondoka. Nitamtukuza Bwana nyakati zote, sifa zake zitakuwa midomoni mwangu siku zote.
大衛在亞比米勒面前裝瘋,被他趕出去,就作這詩。 我要時時稱頌耶和華; 讚美他的話必常在我口中。
2 Nafsi yangu itajisifu katika Bwana, walioonewa watasikia na wafurahi.
我的心必因耶和華誇耀; 謙卑人聽見就要喜樂。
3 Mtukuzeni Bwana pamoja nami, naam, na tulitukuze jina lake pamoja.
你們和我當稱耶和華為大, 一同高舉他的名。
4 Nilimtafuta Bwana naye akanijibu, akaniokoa kwenye hofu zangu zote.
我曾尋求耶和華,他就應允我, 救我脫離了一切的恐懼。
5 Wale wamtazamao hutiwa nuru, nyuso zao hazifunikwi na aibu kamwe.
凡仰望他的,便有光榮; 他們的臉必不蒙羞。
6 Maskini huyu alimwita Bwana, naye akamsikia, akamwokoa katika taabu zake zote.
我這困苦人呼求,耶和華便垂聽, 救我脫離一切患難。
7 Malaika wa Bwana hufanya kituo akiwazunguka wale wamchao, naye huwaokoa.
耶和華的使者在敬畏他的人四圍安營, 搭救他們。
8 Onjeni mwone kwamba Bwana ni mwema, heri mtu yule anayemkimbilia.
你們要嘗嘗主恩的滋味,便知道他是美善; 投靠他的人有福了!
9 Mcheni Bwana enyi watakatifu wake, kwa maana wale wamchao hawapungukiwi na chochote.
耶和華的聖民哪,你們當敬畏他, 因敬畏他的一無所缺。
10 Wana simba wenye nguvu hutindikiwa na kuona njaa, bali wale wamtafutao Bwana hawatakosa kitu chochote kilicho chema.
少壯獅子還缺食忍餓, 但尋求耶和華的甚麼好處都不缺。
11 Njooni, watoto wangu, mnisikilize, nitawafundisha kumcha Bwana.
眾弟子啊,你們當來聽我的話! 我要將敬畏耶和華的道教訓你們。
12 Yeyote kati yenu anayependa uzima na kutamani kuziona siku nyingi njema,
有何人喜好存活, 愛慕長壽,得享美福,
13 basi auzuie ulimi wake na mabaya, na midomo yake kutokana na kusema uongo.
就要禁止舌頭不出惡言, 嘴唇不說詭詐的話。
14 Aache uovu, atende mema, aitafute amani na kuifuatilia.
要離惡行善, 尋求和睦,一心追趕。
15 Macho ya Bwana huwaelekea wenye haki, na masikio yake yako makini kusikiliza kilio chao.
耶和華的眼目看顧義人; 他的耳朵聽他們的呼求。
16 Uso wa Bwana uko kinyume na watendao maovu, ili kufuta kumbukumbu lao duniani.
耶和華向行惡的人變臉, 要從世上除滅他們的名號。
17 Wenye haki hulia, naye Bwana huwasikia, huwaokoa katika taabu zao zote.
義人呼求,耶和華聽見了, 便救他們脫離一切患難。
18 Bwana yu karibu na waliovunjika moyo, na huwaokoa waliopondeka roho.
耶和華靠近傷心的人, 拯救靈性痛悔的人。
19 Mwenye haki ana mateso mengi, lakini Bwana humwokoa nayo yote,
義人多有苦難, 但耶和華救他脫離這一切,
20 huhifadhi mifupa yake yote, hata mmoja hautavunjika.
又保全他一身的骨頭, 連一根也不折斷。
21 Ubaya utamuua mtu mwovu, nao adui za mwenye haki watahukumiwa.
惡必害死惡人; 恨惡義人的,必被定罪。
22 Bwana huwakomboa watumishi wake, yeyote anayemkimbilia yeye hatahukumiwa kamwe.
耶和華救贖他僕人的靈魂; 凡投靠他的,必不致定罪。

< Zaburi 34 >