< Zaburi 33 >

1 Mwimbieni Bwana kwa furaha, enyi wenye haki; kusifu kunawapasa wanyofu wa moyo.
Regozijai-vos no Senhor, vós, justos, pois aos retos convém o louvor.
2 Msifuni Bwana kwa kinubi, mwimbieni sifa kwa zeze la nyuzi kumi.
Louvai ao Senhor com harpa, cantai a ele com saltério de dez cordas.
3 Mwimbieni wimbo mpya; pigeni kwa ustadi, na mpaze sauti za shangwe.
Cantai-lhe um cântico novo: tocai bem e com júbilo.
4 Maana neno la Bwana ni haki na kweli, ni mwaminifu kwa yote atendayo.
Porque a palavra do Senhor é reta, e todas as suas obras são fieis.
5 Bwana hupenda uadilifu na haki; dunia imejaa upendo wake usiokoma.
Ele ama a justiça e o juízo: a terra está cheia da bondade do Senhor.
6 Kwa neno la Bwana mbingu ziliumbwa, jeshi lao la angani kwa pumzi ya kinywa chake.
Pela palavra do Senhor foram feitos os céus, e todo o exército deles pelo espírito da sua boca.
7 Ameyakusanya maji ya bahari kama kwenye chungu; vilindi vya bahari ameviweka katika ghala.
Ele ajunta as águas do mar como num montão; põe os abismos em tesouros.
8 Dunia yote na imwogope Bwana, watu wote wa dunia wamche.
Tema toda a terra ao Senhor; temam-no todos os moradores do mundo.
9 Kwa maana Mungu alisema, na ikawa, aliamuru na ikasimama imara.
Porque falou, e foi feito: mandou, e logo apareceu.
10 Bwana huzuia mipango ya mataifa, hupinga makusudi ya mataifa.
O Senhor desfaz o conselho das nações, quebranta os intentos dos povos.
11 Lakini mipango ya Bwana inasimama imara milele, makusudi ya moyo wake kwa vizazi vyote.
O conselho do Senhor permanece para sempre: os intentos do seu coração de geração em geração.
12 Heri taifa ambalo Bwana ni Mungu wao, watu ambao aliwachagua kuwa urithi wake.
Benaventurada é a nação cujo Deus é o Senhor, e o povo ao qual escolheu para sua herança.
13 Kutoka mbinguni Bwana hutazama chini na kuwaona wanadamu wote;
O Senhor olha desde os céus e está vendo a todos os filhos dos homens.
14 kutoka maskani mwake huwaangalia wote wakaao duniani:
Do lugar da sua habitação contempla todos os moradores da terra,
15 yeye ambaye huumba mioyo yao wote, ambaye huangalia kila kitu wanachokitenda.
Aquele que forma o coração de todos eles, que contempla todas as suas obras.
16 Hakuna mfalme aokokaye kwa ukubwa wa jeshi lake; hakuna shujaa aokokaye kwa wingi wa nguvu zake.
Não há rei que se salve com a grandeza dum exército, nem o homem valente se livra pela muita força.
17 Farasi ni tumaini la bure kwa wokovu, licha ya nguvu zake nyingi, hawezi kuokoa.
O cavalo é falaz para a segurança: não livra ninguém com a sua grande força.
18 Lakini macho ya Bwana yako kwa wale wamchao, kwa wale tumaini lao liko katika upendo wake usio na kikomo,
Eis que os olhos do Senhor estão sobre os que o temem, sobre os que esperam na sua misericórdia;
19 ili awaokoe na mauti, na kuwahifadhi wakati wa njaa.
Para lhes livrar as almas da morte, e para os conservar vivos na fome.
20 Sisi tunamngojea Bwana kwa matumaini, yeye ni msaada wetu na ngao yetu.
A nossa alma espera no Senhor: ele é o nosso auxílio e o nosso escudo.
21 Mioyo yetu humshangilia, kwa maana tunalitumainia jina lake takatifu.
Pois nele se alegra o nosso coração; porquanto temos confiado no seu santo nome.
22 Upendo wako usio na mwisho ukae juu yetu, Ee Bwana, tunapoliweka tumaini letu kwako.
Seja a tua misericórdia, Senhor, sobre nós, como em ti esperamos.

< Zaburi 33 >