< Zaburi 33 >
1 Mwimbieni Bwana kwa furaha, enyi wenye haki; kusifu kunawapasa wanyofu wa moyo.
Regozijae-vos no Senhor, vós, justos, pois aos rectos convem o louvor.
2 Msifuni Bwana kwa kinubi, mwimbieni sifa kwa zeze la nyuzi kumi.
Louvae ao Senhor com harpa, cantae a elle com psalterio de dez cordas.
3 Mwimbieni wimbo mpya; pigeni kwa ustadi, na mpaze sauti za shangwe.
Cantae-lhe um cantico novo: tocae bem e com jubilo.
4 Maana neno la Bwana ni haki na kweli, ni mwaminifu kwa yote atendayo.
Porque a palavra do Senhor é recta, e todas as suas obras são fieis.
5 Bwana hupenda uadilifu na haki; dunia imejaa upendo wake usiokoma.
Elle ama a justiça e o juizo: a terra está cheia da bondade do Senhor.
6 Kwa neno la Bwana mbingu ziliumbwa, jeshi lao la angani kwa pumzi ya kinywa chake.
Pela palavra do Senhor foram feitos os céus, e todo o exercito d'elles pelo espirito da sua bocca.
7 Ameyakusanya maji ya bahari kama kwenye chungu; vilindi vya bahari ameviweka katika ghala.
Elle ajunta as aguas do mar como n'um montão; põe os abysmos em thesouros.
8 Dunia yote na imwogope Bwana, watu wote wa dunia wamche.
Tema toda a terra ao Senhor; temam-n'o todos os moradores do mundo.
9 Kwa maana Mungu alisema, na ikawa, aliamuru na ikasimama imara.
Porque fallou, e foi feito: mandou, e logo appareceu.
10 Bwana huzuia mipango ya mataifa, hupinga makusudi ya mataifa.
O Senhor desfaz o conselho das nações, quebranta os intentos dos povos.
11 Lakini mipango ya Bwana inasimama imara milele, makusudi ya moyo wake kwa vizazi vyote.
O conselho do Senhor permanece para sempre: os intentos do seu coração de geração em geração.
12 Heri taifa ambalo Bwana ni Mungu wao, watu ambao aliwachagua kuwa urithi wake.
Bemaventurada é a nação cujo Deus é o Senhor, e o povo ao qual escolheu para sua herança.
13 Kutoka mbinguni Bwana hutazama chini na kuwaona wanadamu wote;
O Senhor olha desde os céus e está vendo a todos os filhos dos homens.
14 kutoka maskani mwake huwaangalia wote wakaao duniani:
Do logar da sua habitação contempla todos os moradores da terra,
15 yeye ambaye huumba mioyo yao wote, ambaye huangalia kila kitu wanachokitenda.
Aquelle que forma o coração de todos elles, que contempla todas as suas obras.
16 Hakuna mfalme aokokaye kwa ukubwa wa jeshi lake; hakuna shujaa aokokaye kwa wingi wa nguvu zake.
Não ha rei que se salve com a grandeza d'um exercito, nem o homem valente se livra pela muita força.
17 Farasi ni tumaini la bure kwa wokovu, licha ya nguvu zake nyingi, hawezi kuokoa.
O cavallo é fallaz para a segurança: não livra ninguem com a sua grande força.
18 Lakini macho ya Bwana yako kwa wale wamchao, kwa wale tumaini lao liko katika upendo wake usio na kikomo,
Eis que os olhos do Senhor estão sobre os que o temem, sobre os que esperam na sua misericordia;
19 ili awaokoe na mauti, na kuwahifadhi wakati wa njaa.
Para lhes livrar as almas da morte, e para os conservar vivos na fome.
20 Sisi tunamngojea Bwana kwa matumaini, yeye ni msaada wetu na ngao yetu.
A nossa alma espera no Senhor: elle é o nosso auxilio e o nosso escudo.
21 Mioyo yetu humshangilia, kwa maana tunalitumainia jina lake takatifu.
Pois n'elle se alegra o nosso coração; porquanto temos confiado no seu sancto nome.
22 Upendo wako usio na mwisho ukae juu yetu, Ee Bwana, tunapoliweka tumaini letu kwako.
Seja a tua misericordia, Senhor, sobre nós, como em ti esperamos.