< Zaburi 33 >
1 Mwimbieni Bwana kwa furaha, enyi wenye haki; kusifu kunawapasa wanyofu wa moyo.
Psalmus David. Exultate iusti in Domino: rectos decet collaudatio.
2 Msifuni Bwana kwa kinubi, mwimbieni sifa kwa zeze la nyuzi kumi.
Confitemini Domino in cithara: in psalterio decem chordarum psallite illi.
3 Mwimbieni wimbo mpya; pigeni kwa ustadi, na mpaze sauti za shangwe.
Cantate ei canticum novum: bene psallite ei in vociferatione.
4 Maana neno la Bwana ni haki na kweli, ni mwaminifu kwa yote atendayo.
Quia rectum est verbum Domini, et omnia opera eius in fide.
5 Bwana hupenda uadilifu na haki; dunia imejaa upendo wake usiokoma.
Diligit misericordiam et iudicium: misericordia Domini plena est terra.
6 Kwa neno la Bwana mbingu ziliumbwa, jeshi lao la angani kwa pumzi ya kinywa chake.
Verbo Domini caeli firmati sunt: et spiritu oris eius omnis virtus eorum.
7 Ameyakusanya maji ya bahari kama kwenye chungu; vilindi vya bahari ameviweka katika ghala.
Congregans sicut in utre aquas maris: ponens in thesauris abyssos.
8 Dunia yote na imwogope Bwana, watu wote wa dunia wamche.
Timeat Dominum omnis terra: ab eo autem commoveantur omnes inhabitantes orbem.
9 Kwa maana Mungu alisema, na ikawa, aliamuru na ikasimama imara.
Quoniam ipse dixit, et facta sunt: ipse mandavit, et creata sunt.
10 Bwana huzuia mipango ya mataifa, hupinga makusudi ya mataifa.
Dominus dissipat consilia gentium: reprobat autem cogitationes populorum, et reprobat consilia principum.
11 Lakini mipango ya Bwana inasimama imara milele, makusudi ya moyo wake kwa vizazi vyote.
Consilium autem Domini in aeternum manet: cogitationes cordis eius in generatione et generationem.
12 Heri taifa ambalo Bwana ni Mungu wao, watu ambao aliwachagua kuwa urithi wake.
Beata gens, cuius est Dominus, Deus eius: populus, quem elegit in hereditatem sibi.
13 Kutoka mbinguni Bwana hutazama chini na kuwaona wanadamu wote;
De caelo respexit Dominus: vidit omnes filios hominum.
14 kutoka maskani mwake huwaangalia wote wakaao duniani:
De praeparato habitaculo suo respexit super omnes, qui habitant terram.
15 yeye ambaye huumba mioyo yao wote, ambaye huangalia kila kitu wanachokitenda.
Qui finxit sigillatim corda eorum: qui intelligit omnia opera eorum.
16 Hakuna mfalme aokokaye kwa ukubwa wa jeshi lake; hakuna shujaa aokokaye kwa wingi wa nguvu zake.
Non salvatur rex per multam virtutem: et gigas non salvabitur in multitudine virtutis suae.
17 Farasi ni tumaini la bure kwa wokovu, licha ya nguvu zake nyingi, hawezi kuokoa.
Fallax equus ad salutem: in abundantia autem virtutis suae non salvabitur.
18 Lakini macho ya Bwana yako kwa wale wamchao, kwa wale tumaini lao liko katika upendo wake usio na kikomo,
Ecce oculi Domini super metuentes eum: et in eis, qui sperant super misericordia eius.
19 ili awaokoe na mauti, na kuwahifadhi wakati wa njaa.
Ut eruat a morte animas eorum: et alat eos in fame.
20 Sisi tunamngojea Bwana kwa matumaini, yeye ni msaada wetu na ngao yetu.
Anima nostra sustinet Dominum: quoniam adiutor et protector noster est.
21 Mioyo yetu humshangilia, kwa maana tunalitumainia jina lake takatifu.
Quia in eo laetabitur cor nostrum: et in nomine sancto eius speravimus.
22 Upendo wako usio na mwisho ukae juu yetu, Ee Bwana, tunapoliweka tumaini letu kwako.
Fiat misericordia tua Domine super nos: quemadmodum speravimus in te.