< Zaburi 33 >

1 Mwimbieni Bwana kwa furaha, enyi wenye haki; kusifu kunawapasa wanyofu wa moyo.
Jauchzet dem HERRN, ihr Gerechten! Den Redlichen ziemt Lobgesang.
2 Msifuni Bwana kwa kinubi, mwimbieni sifa kwa zeze la nyuzi kumi.
Preiset den HERRN mit der Harfe, spielet ihm auf dem zehnsaitigen Psalter;
3 Mwimbieni wimbo mpya; pigeni kwa ustadi, na mpaze sauti za shangwe.
singet ihm ein neues Lied, spielet gut, mit Posaunenschall!
4 Maana neno la Bwana ni haki na kweli, ni mwaminifu kwa yote atendayo.
Denn das Wort des HERRN ist richtig, und all sein Werk ist Treue.
5 Bwana hupenda uadilifu na haki; dunia imejaa upendo wake usiokoma.
Er liebt Gerechtigkeit und Gericht; die Erde ist voll der Gnade des HERRN.
6 Kwa neno la Bwana mbingu ziliumbwa, jeshi lao la angani kwa pumzi ya kinywa chake.
Die Himmel sind durch das Wort des HERRN gemacht und ihr ganzes Heer durch den Geist seines Mundes.
7 Ameyakusanya maji ya bahari kama kwenye chungu; vilindi vya bahari ameviweka katika ghala.
Er türmt die Meereswellen auf und sammelt Wasservorräte an.
8 Dunia yote na imwogope Bwana, watu wote wa dunia wamche.
Alle Welt fürchte den HERRN, und vor ihm scheue sich alles, was auf dem Erdboden wohnt.
9 Kwa maana Mungu alisema, na ikawa, aliamuru na ikasimama imara.
Denn er sprach, und es geschah; er gebot, und es stand da!
10 Bwana huzuia mipango ya mataifa, hupinga makusudi ya mataifa.
Der HERR vereitelt den Rat der Heiden, er verhindert die Anschläge der Völker.
11 Lakini mipango ya Bwana inasimama imara milele, makusudi ya moyo wake kwa vizazi vyote.
Der Rat des HERRN besteht ewiglich, seines Herzens Gedanken für und für.
12 Heri taifa ambalo Bwana ni Mungu wao, watu ambao aliwachagua kuwa urithi wake.
Wohl dem Volk, dessen Gott der HERR ist, dem Volk, das er sich zum Erbe erwählt hat!
13 Kutoka mbinguni Bwana hutazama chini na kuwaona wanadamu wote;
Vom Himmel schaut der HERR herab, er betrachtet alle Menschenkinder;
14 kutoka maskani mwake huwaangalia wote wakaao duniani:
von seinem festen Thron sieht er alle, die auf Erden wohnen;
15 yeye ambaye huumba mioyo yao wote, ambaye huangalia kila kitu wanachokitenda.
er, der ihrer aller Herz gebildet hat, bemerkt auch alle ihre Werke.
16 Hakuna mfalme aokokaye kwa ukubwa wa jeshi lake; hakuna shujaa aokokaye kwa wingi wa nguvu zake.
Einem König ist nicht geholfen mit viel Heeresmacht, ein Held wird nicht errettet durch große Kraft;
17 Farasi ni tumaini la bure kwa wokovu, licha ya nguvu zake nyingi, hawezi kuokoa.
das Roß ist unzuverlässig zur Rettung, und trotz seiner großen Stärke kann man nicht entrinnen.
18 Lakini macho ya Bwana yako kwa wale wamchao, kwa wale tumaini lao liko katika upendo wake usio na kikomo,
Siehe, der HERR hat ein Auge auf die, so ihn fürchten, die auf seine Gnade hoffen,
19 ili awaokoe na mauti, na kuwahifadhi wakati wa njaa.
daß er ihre Seele vom Tode errette und sie in der Teuerung am Leben erhalte.
20 Sisi tunamngojea Bwana kwa matumaini, yeye ni msaada wetu na ngao yetu.
Unsre Seele harrt auf den HERRN; er ist unsre Hilfe und unser Schild.
21 Mioyo yetu humshangilia, kwa maana tunalitumainia jina lake takatifu.
Ja, an ihm soll unser Herz sich freuen; denn auf seinen heiligen Namen haben wir unser Vertrauen gesetzt.
22 Upendo wako usio na mwisho ukae juu yetu, Ee Bwana, tunapoliweka tumaini letu kwako.
Deine Gnade, o HERR, sei über uns, wie wir es von dir erhoffen!

< Zaburi 33 >