< Zaburi 33 >
1 Mwimbieni Bwana kwa furaha, enyi wenye haki; kusifu kunawapasa wanyofu wa moyo.
Justes, réjouissez-vous en l’Éternel! La louange sied aux hommes droits.
2 Msifuni Bwana kwa kinubi, mwimbieni sifa kwa zeze la nyuzi kumi.
Célébrez l’Éternel avec la harpe, Célébrez-le sur le luth à dix cordes.
3 Mwimbieni wimbo mpya; pigeni kwa ustadi, na mpaze sauti za shangwe.
Chantez-lui un cantique nouveau! Faites retentir vos instruments et vos voix!
4 Maana neno la Bwana ni haki na kweli, ni mwaminifu kwa yote atendayo.
Car la parole de l’Éternel est droite, Et toutes ses œuvres s’accomplissent avec fidélité;
5 Bwana hupenda uadilifu na haki; dunia imejaa upendo wake usiokoma.
Il aime la justice et la droiture; La bonté de l’Éternel remplit la terre.
6 Kwa neno la Bwana mbingu ziliumbwa, jeshi lao la angani kwa pumzi ya kinywa chake.
Les cieux ont été faits par la parole de l’Éternel, Et toute leur armée par le souffle de sa bouche.
7 Ameyakusanya maji ya bahari kama kwenye chungu; vilindi vya bahari ameviweka katika ghala.
Il amoncelle en un tas les eaux de la mer, Il met dans des réservoirs les abîmes.
8 Dunia yote na imwogope Bwana, watu wote wa dunia wamche.
Que toute la terre craigne l’Éternel! Que tous les habitants du monde tremblent devant lui!
9 Kwa maana Mungu alisema, na ikawa, aliamuru na ikasimama imara.
Car il dit, et la chose arrive; Il ordonne, et elle existe.
10 Bwana huzuia mipango ya mataifa, hupinga makusudi ya mataifa.
L’Éternel renverse les desseins des nations, Il anéantit les projets des peuples;
11 Lakini mipango ya Bwana inasimama imara milele, makusudi ya moyo wake kwa vizazi vyote.
Les desseins de l’Éternel subsistent à toujours, Et les projets de son cœur, de génération en génération.
12 Heri taifa ambalo Bwana ni Mungu wao, watu ambao aliwachagua kuwa urithi wake.
Heureuse la nation dont l’Éternel est le Dieu! Heureux le peuple qu’il choisit pour son héritage!
13 Kutoka mbinguni Bwana hutazama chini na kuwaona wanadamu wote;
L’Éternel regarde du haut des cieux, Il voit tous les fils de l’homme;
14 kutoka maskani mwake huwaangalia wote wakaao duniani:
Du lieu de sa demeure il observe Tous les habitants de la terre,
15 yeye ambaye huumba mioyo yao wote, ambaye huangalia kila kitu wanachokitenda.
Lui qui forme leur cœur à tous, Qui est attentif à toutes leurs actions.
16 Hakuna mfalme aokokaye kwa ukubwa wa jeshi lake; hakuna shujaa aokokaye kwa wingi wa nguvu zake.
Ce n’est pas une grande armée qui sauve le roi, Ce n’est pas une grande force qui délivre le héros;
17 Farasi ni tumaini la bure kwa wokovu, licha ya nguvu zake nyingi, hawezi kuokoa.
Le cheval est impuissant pour assurer le salut, Et toute sa vigueur ne donne pas la délivrance.
18 Lakini macho ya Bwana yako kwa wale wamchao, kwa wale tumaini lao liko katika upendo wake usio na kikomo,
Voici, l’œil de l’Éternel est sur ceux qui le craignent, Sur ceux qui espèrent en sa bonté,
19 ili awaokoe na mauti, na kuwahifadhi wakati wa njaa.
Afin d’arracher leur âme à la mort Et de les faire vivre au milieu de la famine.
20 Sisi tunamngojea Bwana kwa matumaini, yeye ni msaada wetu na ngao yetu.
Notre âme espère en l’Éternel; Il est notre secours et notre bouclier.
21 Mioyo yetu humshangilia, kwa maana tunalitumainia jina lake takatifu.
Car notre cœur met en lui sa joie, Car nous avons confiance en son saint nom.
22 Upendo wako usio na mwisho ukae juu yetu, Ee Bwana, tunapoliweka tumaini letu kwako.
Éternel! Que ta grâce soit sur nous, Comme nous espérons en toi!