< Zaburi 33 >
1 Mwimbieni Bwana kwa furaha, enyi wenye haki; kusifu kunawapasa wanyofu wa moyo.
Shout for joy in the Lord, you righteous: praise for the upright is seemly.
2 Msifuni Bwana kwa kinubi, mwimbieni sifa kwa zeze la nyuzi kumi.
Give thanks to the Lord on the lyre, play to him on a ten-stringed harp.
3 Mwimbieni wimbo mpya; pigeni kwa ustadi, na mpaze sauti za shangwe.
Sing to him a new song, play skilfully and shout merrily.
4 Maana neno la Bwana ni haki na kweli, ni mwaminifu kwa yote atendayo.
For the Lord is straight in his promise; and all that he does is in faithfulness.
5 Bwana hupenda uadilifu na haki; dunia imejaa upendo wake usiokoma.
Justice and right he loves; the earth is full of his kindness.
6 Kwa neno la Bwana mbingu ziliumbwa, jeshi lao la angani kwa pumzi ya kinywa chake.
By his word the heavens were made, all their host by the breath of his mouth.
7 Ameyakusanya maji ya bahari kama kwenye chungu; vilindi vya bahari ameviweka katika ghala.
He gathers the sea in a bottle, the ocean he puts into store-houses.
8 Dunia yote na imwogope Bwana, watu wote wa dunia wamche.
Let the whole world honor the Lord, let all who live on earth be in awe.
9 Kwa maana Mungu alisema, na ikawa, aliamuru na ikasimama imara.
For at his word it came into being, at his command it stood forth.
10 Bwana huzuia mipango ya mataifa, hupinga makusudi ya mataifa.
The Lord frustrates the designs of the nations, what the peoples have purposed, he brings to nought,
11 Lakini mipango ya Bwana inasimama imara milele, makusudi ya moyo wake kwa vizazi vyote.
but the Lord’s own design will stand forever, and what his heart has purposed, through all generations.
12 Heri taifa ambalo Bwana ni Mungu wao, watu ambao aliwachagua kuwa urithi wake.
Happy the nation whose God is the Lord, the people he chose for himself as his own.
13 Kutoka mbinguni Bwana hutazama chini na kuwaona wanadamu wote;
The Lord looks down from heaven, he sees all of humanity;
14 kutoka maskani mwake huwaangalia wote wakaao duniani:
from where he rules he gazes on all who inhabit the earth.
15 yeye ambaye huumba mioyo yao wote, ambaye huangalia kila kitu wanachokitenda.
He fashions the hearts of them all, and gives heed to all that they do.
16 Hakuna mfalme aokokaye kwa ukubwa wa jeshi lake; hakuna shujaa aokokaye kwa wingi wa nguvu zake.
It is not by great armies that kings are victorious, it is not by great strength that a warrior saves himself;
17 Farasi ni tumaini la bure kwa wokovu, licha ya nguvu zake nyingi, hawezi kuokoa.
false hope is the war-horse to usher in victory, for all its great might it can provide no escape.
18 Lakini macho ya Bwana yako kwa wale wamchao, kwa wale tumaini lao liko katika upendo wake usio na kikomo,
See! The eye of the Lord is on those who fear him, on those who hope in his kindness;
19 ili awaokoe na mauti, na kuwahifadhi wakati wa njaa.
to deliver their life from death, and to keep them alive in famine.
20 Sisi tunamngojea Bwana kwa matumaini, yeye ni msaada wetu na ngao yetu.
We wait for the Lord: he is our help and our shield.
21 Mioyo yetu humshangilia, kwa maana tunalitumainia jina lake takatifu.
For in him our heart is glad, we trust in his holy name.
22 Upendo wako usio na mwisho ukae juu yetu, Ee Bwana, tunapoliweka tumaini letu kwako.
Let your kindness, O Lord, be upon us, as is our hope in you.