< Zaburi 33 >

1 Mwimbieni Bwana kwa furaha, enyi wenye haki; kusifu kunawapasa wanyofu wa moyo.
Rejoice in the LORD, you righteous. Praise is fitting for the upright.
2 Msifuni Bwana kwa kinubi, mwimbieni sifa kwa zeze la nyuzi kumi.
Give thanks to the LORD with the lyre. Sing praises to him with the harp of ten strings.
3 Mwimbieni wimbo mpya; pigeni kwa ustadi, na mpaze sauti za shangwe.
Sing to him a new song. Play skillfully with a shout of joy.
4 Maana neno la Bwana ni haki na kweli, ni mwaminifu kwa yote atendayo.
For the word of the LORD is right. All his work is done in faithfulness.
5 Bwana hupenda uadilifu na haki; dunia imejaa upendo wake usiokoma.
He loves righteousness and justice. The earth is full of the loving kindness of the LORD.
6 Kwa neno la Bwana mbingu ziliumbwa, jeshi lao la angani kwa pumzi ya kinywa chake.
By the word of the LORD the heavens were made; and all their host by the breath of his mouth.
7 Ameyakusanya maji ya bahari kama kwenye chungu; vilindi vya bahari ameviweka katika ghala.
He gathers the waters of the sea together as a heap. He lays up the deeps in storehouses.
8 Dunia yote na imwogope Bwana, watu wote wa dunia wamche.
Let all the earth fear the LORD. Let all the inhabitants of the world stand in awe of him.
9 Kwa maana Mungu alisema, na ikawa, aliamuru na ikasimama imara.
For he spoke, and it was done. He commanded, and it stood firm.
10 Bwana huzuia mipango ya mataifa, hupinga makusudi ya mataifa.
The LORD nullifies the counsel of the nations. He makes the thoughts of the peoples to be of no effect.
11 Lakini mipango ya Bwana inasimama imara milele, makusudi ya moyo wake kwa vizazi vyote.
The counsel of the LORD stands fast forever, the thoughts of his heart to all generations.
12 Heri taifa ambalo Bwana ni Mungu wao, watu ambao aliwachagua kuwa urithi wake.
Blessed is the nation whose God is the LORD, the people whom he has chosen for his own inheritance.
13 Kutoka mbinguni Bwana hutazama chini na kuwaona wanadamu wote;
The LORD looks from heaven. He sees all the descendants of Adam.
14 kutoka maskani mwake huwaangalia wote wakaao duniani:
From the place of his habitation he looks out on all the inhabitants of the earth,
15 yeye ambaye huumba mioyo yao wote, ambaye huangalia kila kitu wanachokitenda.
he who fashions all of their hearts; and he considers all of their works.
16 Hakuna mfalme aokokaye kwa ukubwa wa jeshi lake; hakuna shujaa aokokaye kwa wingi wa nguvu zake.
There is no king saved by the multitude of an army. A mighty man is not delivered by great strength.
17 Farasi ni tumaini la bure kwa wokovu, licha ya nguvu zake nyingi, hawezi kuokoa.
A horse is a vain thing for safety, neither does he deliver any by his great power.
18 Lakini macho ya Bwana yako kwa wale wamchao, kwa wale tumaini lao liko katika upendo wake usio na kikomo,
Look, the LORD's eye is on those who fear him, on those who hope in his loving kindness;
19 ili awaokoe na mauti, na kuwahifadhi wakati wa njaa.
to deliver their soul from death, to keep them alive in famine.
20 Sisi tunamngojea Bwana kwa matumaini, yeye ni msaada wetu na ngao yetu.
Our soul waits for the LORD. He is our help and our shield.
21 Mioyo yetu humshangilia, kwa maana tunalitumainia jina lake takatifu.
For our heart rejoices in him, because we have trusted in his holy name.
22 Upendo wako usio na mwisho ukae juu yetu, Ee Bwana, tunapoliweka tumaini letu kwako.
Let your loving kindness be on us, LORD, since we have hoped in you.

< Zaburi 33 >