< Zaburi 33 >

1 Mwimbieni Bwana kwa furaha, enyi wenye haki; kusifu kunawapasa wanyofu wa moyo.
Gij rechtvaardigen, heft Jahweh een jubelzang aan; De psalm is een lust voor de vromen!
2 Msifuni Bwana kwa kinubi, mwimbieni sifa kwa zeze la nyuzi kumi.
Looft Jahweh met citers, Bespeelt voor Hem de tiensnarige harp;
3 Mwimbieni wimbo mpya; pigeni kwa ustadi, na mpaze sauti za shangwe.
Stemt een nieuw lied voor Hem aan, Tokkelt de lieren, lustig en luid!
4 Maana neno la Bwana ni haki na kweli, ni mwaminifu kwa yote atendayo.
Want Jahweh’s woord is waarachtig, Onveranderlijk al zijn daden.
5 Bwana hupenda uadilifu na haki; dunia imejaa upendo wake usiokoma.
Gerechtigheid en recht heeft Hij lief; Van Jahweh’s goedheid is de aarde vol.
6 Kwa neno la Bwana mbingu ziliumbwa, jeshi lao la angani kwa pumzi ya kinywa chake.
Door het woord van Jahweh zijn de hemelen gemaakt, Door de adem van zijn mond heel hun heir;
7 Ameyakusanya maji ya bahari kama kwenye chungu; vilindi vya bahari ameviweka katika ghala.
Hij verzamelde het water der zee in een zak, Legde de oceanen in schuren op.
8 Dunia yote na imwogope Bwana, watu wote wa dunia wamche.
Heel de aarde moet Jahweh vrezen, Al de bewoners der wereld Hem duchten.
9 Kwa maana Mungu alisema, na ikawa, aliamuru na ikasimama imara.
Want Hij sprak: en het was; Hij gebood: en het stond.
10 Bwana huzuia mipango ya mataifa, hupinga makusudi ya mataifa.
De raadslagen der volken gooit Jahweh omver, Hij verijdelt de plannen der naties;
11 Lakini mipango ya Bwana inasimama imara milele, makusudi ya moyo wake kwa vizazi vyote.
Maar Jahweh’s raadsbesluit staat in eeuwigheid vast: Wat zijn hart heeft bedacht, van geslacht tot geslacht.
12 Heri taifa ambalo Bwana ni Mungu wao, watu ambao aliwachagua kuwa urithi wake.
Gelukkig de natie, die Jahweh tot God heeft, Het volk, dat Hij Zich tot erfdeel verkoos!
13 Kutoka mbinguni Bwana hutazama chini na kuwaona wanadamu wote;
Jahweh ziet neer uit de hemel, Richt zijn blik op alle kinderen der mensen.
14 kutoka maskani mwake huwaangalia wote wakaao duniani:
Hij let van de plaats, waar Hij troont, Op alle bewoners der aarde:
15 yeye ambaye huumba mioyo yao wote, ambaye huangalia kila kitu wanachokitenda.
Hij, die aller hart heeft geschapen, En al hun daden doorgrondt.
16 Hakuna mfalme aokokaye kwa ukubwa wa jeshi lake; hakuna shujaa aokokaye kwa wingi wa nguvu zake.
Geen koning overwint door de macht van zijn heir, Geen held wordt gered door geweldige kracht;
17 Farasi ni tumaini la bure kwa wokovu, licha ya nguvu zake nyingi, hawezi kuokoa.
Ook het ros kan de zege niet schenken, Door zijn grote snelheid niet redden.
18 Lakini macho ya Bwana yako kwa wale wamchao, kwa wale tumaini lao liko katika upendo wake usio na kikomo,
Maar het oog van Jahweh rust op hen, die Hem vrezen, En die op zijn goedheid vertrouwen:
19 ili awaokoe na mauti, na kuwahifadhi wakati wa njaa.
Om ze te redden van de dood, Ze in het leven te houden bij hongersnood.
20 Sisi tunamngojea Bwana kwa matumaini, yeye ni msaada wetu na ngao yetu.
Onze ziel blijft opzien tot Jahweh: Hij is onze hulp en ons schild;
21 Mioyo yetu humshangilia, kwa maana tunalitumainia jina lake takatifu.
In Hem verheugt zich ons hart, Wij vertrouwen op zijn heilige Naam.
22 Upendo wako usio na mwisho ukae juu yetu, Ee Bwana, tunapoliweka tumaini letu kwako.
Uw genade, o Jahweh, dale over ons neer, Naarmate wij op U blijven hopen!

< Zaburi 33 >