< Zaburi 32 >

1 Zaburi ya Daudi. Funzo. Heri mtu yule ambaye amesamehewa makosa yake, ambaye dhambi zake zimefunikwa.
Dāvida pamācīšana. Svētīgs ir tas, kam pārkāpumi piedoti, kam grēki apklāti.
2 Heri mtu yule ambaye Bwana hamhesabii dhambi, na ambaye rohoni mwake hamna udanganyifu.
Svētīgs tas cilvēks, kam Tas Kungs noziegumus nepielīdzina, un kura garā viltības nav.
3 Niliponyamaza, mifupa yangu ilichakaa kwa kulia kwa maumivu makali mchana kutwa.
Kad es klusu cietu, tad panīka mani kauli caur manu kaukšanu cauru dienu.
4 Usiku na mchana mkono wako ulinilemea, nguvu zangu zilinyonywa kama vile katika joto la kiangazi.
Jo Tava roka dienām naktīm bija grūta uz manis, ka mans zaļums nokalta kā vasaras bullā. (Sela)
5 Kisha nilikujulisha dhambi yangu wala sikuficha uovu wangu. Nilisema, “Nitaungama makosa yangu kwa Bwana.” Ndipo uliponisamehe hatia ya dhambi yangu.
Savus grēkus es Tev sūdzu un neapklāju savus noziegumus; es sacīju: es izteikšu Tam Kungam savus pārkāpumus, tad Tu piedevi manu grēku noziegumus. (Sela)
6 Kwa hiyo kila mtu mcha Mungu akuombe wakati unapopatikana, hakika maji makuu yatakapofurika hayatamfikia yeye.
Par to Tevi pielūgs visi svētie īstenā atrašanas laikā; tādēļ jebšu lieli ūdens plūdi nāktu, taču tie tos neaizņems.
7 Wewe ndiwe mahali pangu pa kujificha, utaniepusha na taabu na kunizunguka kwa nyimbo za wokovu.
Tu esi mans patvērums, no bailēm Tu mani pasargāsi; Tu liksi atskanēt ap mani pestīšanas gavilēm. (Sela)
8 Nitakufundisha na kukuonyesha njia utakayoiendea; nitakushauri na kukuangalia.
“Es tev došu saprašanu un tev mācīšu to ceļu, pa kuru jāiet; Es došu padomu, Mana acs būs pār tevi.
9 Usiwe kama farasi au nyumbu wasio na akili, ambao ni lazima waongozwe kwa lijamu na hatamu la sivyo hawatakukaribia.
Neesiet kā zirgi un zirgēzeļi, kam prāta nav, kam iemaukti un laužņi jāliek mutē, kad negrib nākt pie tevis.”
10 Mtu mwovu ana taabu nyingi, bali upendo usio na kikomo wa Bwana unamzunguka mtu anayemtumaini.
Bezdievīgam ir daudz sāpes, bet kas uz To Kungu cer, to žēlastība apkamps.
11 Shangilieni katika Bwana na mfurahi, enyi wenye haki! Imbeni, nyote mlio wanyofu wa moyo!
Priecājaties iekš Tā Kunga un līksmojaties, jūs taisnie, un slavējiet, visi jūs sirds skaidrie.

< Zaburi 32 >