< Zaburi 32 >

1 Zaburi ya Daudi. Funzo. Heri mtu yule ambaye amesamehewa makosa yake, ambaye dhambi zake zimefunikwa.
Maskil (cantique) de David. Heureux celui dont la transgression est pardonnée, et dont le péché est couvert!
2 Heri mtu yule ambaye Bwana hamhesabii dhambi, na ambaye rohoni mwake hamna udanganyifu.
Heureux l'homme à qui l'Éternel n'impute pas l'iniquité, et dans l'esprit duquel il n'y a point de fraude!
3 Niliponyamaza, mifupa yangu ilichakaa kwa kulia kwa maumivu makali mchana kutwa.
Quand je me suis tu, mes os se sont consumés, et je gémissais tout le jour.
4 Usiku na mchana mkono wako ulinilemea, nguvu zangu zilinyonywa kama vile katika joto la kiangazi.
Car, jour et nuit, ta main s'appesantissait sur moi; ma vigueur se changeait en une sécheresse d'été. (Sélah, pause)
5 Kisha nilikujulisha dhambi yangu wala sikuficha uovu wangu. Nilisema, “Nitaungama makosa yangu kwa Bwana.” Ndipo uliponisamehe hatia ya dhambi yangu.
Je t'ai fait connaître mon péché, et je ne t'ai point caché mon iniquité. J'ai dit: Je confesserai mes transgressions à l'Éternel; et tu as ôté la peine de mon péché. (Sélah)
6 Kwa hiyo kila mtu mcha Mungu akuombe wakati unapopatikana, hakika maji makuu yatakapofurika hayatamfikia yeye.
C'est pourquoi tout fidèle t'invoquera au temps qu'on te trouve; et quand les grandes eaux déborderaient, seul il n'en sera pas atteint.
7 Wewe ndiwe mahali pangu pa kujificha, utaniepusha na taabu na kunizunguka kwa nyimbo za wokovu.
Tu es ma retraite; tu me garantis de la détresse, tu m'environnes de chants de délivrance. (Sélah)
8 Nitakufundisha na kukuonyesha njia utakayoiendea; nitakushauri na kukuangalia.
Je te rendrai intelligent, m'a dit l'Éternel, je t'enseignerai le chemin où tu dois marcher; je te conduirai; mon œil sera sur toi.
9 Usiwe kama farasi au nyumbu wasio na akili, ambao ni lazima waongozwe kwa lijamu na hatamu la sivyo hawatakukaribia.
Ne soyez pas comme le cheval et comme le mulet sans intelligence, dont il faut serrer la bouche avec un mors et un frein, de peur qu'ils n'approchent de toi.
10 Mtu mwovu ana taabu nyingi, bali upendo usio na kikomo wa Bwana unamzunguka mtu anayemtumaini.
Beaucoup de douleurs atteindront le méchant; mais la grâce environnera celui qui se confie en l'Éternel.
11 Shangilieni katika Bwana na mfurahi, enyi wenye haki! Imbeni, nyote mlio wanyofu wa moyo!
Justes, réjouissez-vous en l'Éternel, et vous égayez! Chantez de joie, vous tous qui avez le cœur droit!

< Zaburi 32 >