< Zaburi 32 >

1 Zaburi ya Daudi. Funzo. Heri mtu yule ambaye amesamehewa makosa yake, ambaye dhambi zake zimefunikwa.
[A Psalm] of David, Maschil. Blessed [is he whose] transgression [is] forgiven, [whose] sin [is] covered.
2 Heri mtu yule ambaye Bwana hamhesabii dhambi, na ambaye rohoni mwake hamna udanganyifu.
Blessed [is] the man to whom the LORD imputeth not iniquity, and in whose spirit [there is] no guile.
3 Niliponyamaza, mifupa yangu ilichakaa kwa kulia kwa maumivu makali mchana kutwa.
When I kept silence, my bones became old through my roaring all the day long.
4 Usiku na mchana mkono wako ulinilemea, nguvu zangu zilinyonywa kama vile katika joto la kiangazi.
For day and night thy hand was heavy upon me: my moisture is turned into the drouth of summer. (Selah)
5 Kisha nilikujulisha dhambi yangu wala sikuficha uovu wangu. Nilisema, “Nitaungama makosa yangu kwa Bwana.” Ndipo uliponisamehe hatia ya dhambi yangu.
I acknowledged my sin to thee, and my iniquity have I not hid. I said, I will confess my transgressions to the LORD; and thou forgavest the iniquity of my sin. (Selah)
6 Kwa hiyo kila mtu mcha Mungu akuombe wakati unapopatikana, hakika maji makuu yatakapofurika hayatamfikia yeye.
For this shall every one that is godly pray to thee in a time when thou mayest be found: surely in the floods of great waters they shall not come nigh to him.
7 Wewe ndiwe mahali pangu pa kujificha, utaniepusha na taabu na kunizunguka kwa nyimbo za wokovu.
Thou [art] my hiding place; thou wilt preserve me from trouble; thou wilt compass me about with songs of deliverance. (Selah)
8 Nitakufundisha na kukuonyesha njia utakayoiendea; nitakushauri na kukuangalia.
I will instruct thee, and teach thee in the way which thou shalt go: I will guide thee with my eye.
9 Usiwe kama farasi au nyumbu wasio na akili, ambao ni lazima waongozwe kwa lijamu na hatamu la sivyo hawatakukaribia.
Be ye not as the horse, [or] as the mule, [which] have no understanding: whose mouth must be held in with bit and bridle, lest they come near to thee.
10 Mtu mwovu ana taabu nyingi, bali upendo usio na kikomo wa Bwana unamzunguka mtu anayemtumaini.
Many sorrows [shall be] to the wicked: but he that trusteth in the LORD, mercy shall encompass him.
11 Shangilieni katika Bwana na mfurahi, enyi wenye haki! Imbeni, nyote mlio wanyofu wa moyo!
Be glad in the LORD, and rejoice, ye righteous: and shout for joy, all [ye that are] upright in heart.

< Zaburi 32 >