< Zaburi 32 >

1 Zaburi ya Daudi. Funzo. Heri mtu yule ambaye amesamehewa makosa yake, ambaye dhambi zake zimefunikwa.
A psalm of David. A maschil. Blessed is the person whose transgression is forgiven, whose sin is covered.
2 Heri mtu yule ambaye Bwana hamhesabii dhambi, na ambaye rohoni mwake hamna udanganyifu.
Blessed is the man to whom Yahweh reckons no guilt and in whose spirit there is no deceit.
3 Niliponyamaza, mifupa yangu ilichakaa kwa kulia kwa maumivu makali mchana kutwa.
When I remained silent, my bones were wasting away while I groaned all day long.
4 Usiku na mchana mkono wako ulinilemea, nguvu zangu zilinyonywa kama vile katika joto la kiangazi.
For day and night your hand was heavy upon me. My strength withered as in summer drought. (Selah)
5 Kisha nilikujulisha dhambi yangu wala sikuficha uovu wangu. Nilisema, “Nitaungama makosa yangu kwa Bwana.” Ndipo uliponisamehe hatia ya dhambi yangu.
Then I acknowledged my sin to you, and I no longer hid my iniquity. I said, “I will confess my transgressions to Yahweh,” and you forgave the guilt of my sin. (Selah)
6 Kwa hiyo kila mtu mcha Mungu akuombe wakati unapopatikana, hakika maji makuu yatakapofurika hayatamfikia yeye.
Because of this, all who are godly should pray to you at a time of great distress. Then when the surging waters overflow, they will not reach those people.
7 Wewe ndiwe mahali pangu pa kujificha, utaniepusha na taabu na kunizunguka kwa nyimbo za wokovu.
You are my hiding place; you will guard me from trouble. You will surround me with the songs of victory. (Selah)
8 Nitakufundisha na kukuonyesha njia utakayoiendea; nitakushauri na kukuangalia.
I will instruct you and teach you in the way which you should go. I will instruct you with my eye upon you.
9 Usiwe kama farasi au nyumbu wasio na akili, ambao ni lazima waongozwe kwa lijamu na hatamu la sivyo hawatakukaribia.
Do not be like a horse or like a mule, which have no understanding; it is only with bridle and bit to control them that they will go where you want them to.
10 Mtu mwovu ana taabu nyingi, bali upendo usio na kikomo wa Bwana unamzunguka mtu anayemtumaini.
The wicked have many sorrows, but Yahweh's covenant faithfulness will surround the one who trusts in him.
11 Shangilieni katika Bwana na mfurahi, enyi wenye haki! Imbeni, nyote mlio wanyofu wa moyo!
Be glad in Yahweh, and rejoice, you righteous; shout for joy, all you who are upright in heart.

< Zaburi 32 >