< Zaburi 32 >
1 Zaburi ya Daudi. Funzo. Heri mtu yule ambaye amesamehewa makosa yake, ambaye dhambi zake zimefunikwa.
Of David a poem how blessed! [is one who] is forgiven of transgression [is one who] is covered of sin.
2 Heri mtu yule ambaye Bwana hamhesabii dhambi, na ambaye rohoni mwake hamna udanganyifu.
How blessed! [is] a person [whom] not he reckons Yahweh to him iniquity and there not in spirit his [is] deceit.
3 Niliponyamaza, mifupa yangu ilichakaa kwa kulia kwa maumivu makali mchana kutwa.
If I kept silent they became worn out bones my in cry of distress my all the day.
4 Usiku na mchana mkono wako ulinilemea, nguvu zangu zilinyonywa kama vile katika joto la kiangazi.
For - by day and night it was heavy on me hand your it was changed juice my by [the] dry heat of summer (Selah)
5 Kisha nilikujulisha dhambi yangu wala sikuficha uovu wangu. Nilisema, “Nitaungama makosa yangu kwa Bwana.” Ndipo uliponisamehe hatia ya dhambi yangu.
Sin my I made known to you and iniquity my not I covered I said I will confess on transgressions my to Yahweh and you you forgave [the] guilt of sin my (Selah)
6 Kwa hiyo kila mtu mcha Mungu akuombe wakati unapopatikana, hakika maji makuu yatakapofurika hayatamfikia yeye.
On this let him pray every faithful [person] - to you to a time of finding certainly to a flood of waters many to him not they will reach.
7 Wewe ndiwe mahali pangu pa kujificha, utaniepusha na taabu na kunizunguka kwa nyimbo za wokovu.
You - [are] a hiding place of me from distress you will preserve me shouts of deliverance; [surely] you will surround me (Selah)
8 Nitakufundisha na kukuonyesha njia utakayoiendea; nitakushauri na kukuangalia.
I will instruct you - and I will teach you [the] way which you will go I will counsel [you] [will be] on you eye my.
9 Usiwe kama farasi au nyumbu wasio na akili, ambao ni lazima waongozwe kwa lijamu na hatamu la sivyo hawatakukaribia.
May not you be - like a horse like a mule [which] there not [is] understanding with bridle and halter trapping[s] its to restrain not to draw near to you.
10 Mtu mwovu ana taabu nyingi, bali upendo usio na kikomo wa Bwana unamzunguka mtu anayemtumaini.
Many pains [belong] to wicked [person] and the [one who] trusts in Yahweh covenant loyalty it will surround him.
11 Shangilieni katika Bwana na mfurahi, enyi wenye haki! Imbeni, nyote mlio wanyofu wa moyo!
Rejoice in Yahweh and be glad O righteous [people] and shout for joy O all [people] upright of heart.