< Zaburi 32 >
1 Zaburi ya Daudi. Funzo. Heri mtu yule ambaye amesamehewa makosa yake, ambaye dhambi zake zimefunikwa.
Of David. A maskil. Happy those whose transgression is pardoned, whose sin is covered.
2 Heri mtu yule ambaye Bwana hamhesabii dhambi, na ambaye rohoni mwake hamna udanganyifu.
Happy are those, free from falseness of spirit, to whom the Lord reckons no debt of guilt.
3 Niliponyamaza, mifupa yangu ilichakaa kwa kulia kwa maumivu makali mchana kutwa.
When I held my peace, my bones wore away with my endless groaning;
4 Usiku na mchana mkono wako ulinilemea, nguvu zangu zilinyonywa kama vile katika joto la kiangazi.
for day and night did your hand lie heavy upon me. The sap of my life was dried up as with fierce summer-heat. (Selah)
5 Kisha nilikujulisha dhambi yangu wala sikuficha uovu wangu. Nilisema, “Nitaungama makosa yangu kwa Bwana.” Ndipo uliponisamehe hatia ya dhambi yangu.
I began to acknowledge my sin, not concealing my guilt; and the moment I vowed to confess to the Lord my transgression, then you yourself did pardon the guilt of my sin. (Selah)
6 Kwa hiyo kila mtu mcha Mungu akuombe wakati unapopatikana, hakika maji makuu yatakapofurika hayatamfikia yeye.
For this cause let all who are faithful pray to you in the time of distress; then, when the great waters rush, they will not reach to him.
7 Wewe ndiwe mahali pangu pa kujificha, utaniepusha na taabu na kunizunguka kwa nyimbo za wokovu.
For you are my shelter, you protect me from trouble, and surround me with deliverance. (Selah)
8 Nitakufundisha na kukuonyesha njia utakayoiendea; nitakushauri na kukuangalia.
“With my eye steadfastly upon you, I will instruct and teach you The way you should go.
9 Usiwe kama farasi au nyumbu wasio na akili, ambao ni lazima waongozwe kwa lijamu na hatamu la sivyo hawatakukaribia.
Do not be like the horse or the mule, that have no understanding, but need bridle and halter to curb them, else they will not come near to you.”
10 Mtu mwovu ana taabu nyingi, bali upendo usio na kikomo wa Bwana unamzunguka mtu anayemtumaini.
The godless have many sorrows, but those who trust in the Lord will be compassed about by his kindness.
11 Shangilieni katika Bwana na mfurahi, enyi wenye haki! Imbeni, nyote mlio wanyofu wa moyo!
Be glad in the Lord, and rejoice, you righteous; and ring out your joy, all you upright in heart.