< Zaburi 32 >

1 Zaburi ya Daudi. Funzo. Heri mtu yule ambaye amesamehewa makosa yake, ambaye dhambi zake zimefunikwa.
A Psalm of David. Maschil. Happy is he whose transgression is forgiven, whose sin is pardoned.
2 Heri mtu yule ambaye Bwana hamhesabii dhambi, na ambaye rohoni mwake hamna udanganyifu.
Happy is the man unto whom the LORD counteth not iniquity, and in whose spirit there is no guile.
3 Niliponyamaza, mifupa yangu ilichakaa kwa kulia kwa maumivu makali mchana kutwa.
When I kept silence, my bones wore away through my groaning all the day long.
4 Usiku na mchana mkono wako ulinilemea, nguvu zangu zilinyonywa kama vile katika joto la kiangazi.
For day and night Thy hand was heavy upon me; my sap was turned as in the droughts of summer. (Selah)
5 Kisha nilikujulisha dhambi yangu wala sikuficha uovu wangu. Nilisema, “Nitaungama makosa yangu kwa Bwana.” Ndipo uliponisamehe hatia ya dhambi yangu.
I acknowledged my sin unto Thee, and mine iniquity have I not hid; I said: 'I will make confession concerning my transgressions unto the LORD' — and Thou, Thou forgavest the iniquity of my sin. (Selah)
6 Kwa hiyo kila mtu mcha Mungu akuombe wakati unapopatikana, hakika maji makuu yatakapofurika hayatamfikia yeye.
For this let every one that is godly pray unto Thee in a time when Thou mayest be found; surely, when the great waters overflow, they will not reach unto him.
7 Wewe ndiwe mahali pangu pa kujificha, utaniepusha na taabu na kunizunguka kwa nyimbo za wokovu.
Thou art my hiding-place; Thou wilt preserve me from the adversary; with songs of deliverance Thou wilt compass me about. (Selah)
8 Nitakufundisha na kukuonyesha njia utakayoiendea; nitakushauri na kukuangalia.
'I will instruct thee and teach thee in the way which thou shalt go; I will give counsel, Mine eye being upon thee.'
9 Usiwe kama farasi au nyumbu wasio na akili, ambao ni lazima waongozwe kwa lijamu na hatamu la sivyo hawatakukaribia.
Be ye not as the horse, or as the mule, which have no understanding; whose mouth must be held in with bit and bridle, that they come not near unto thee.
10 Mtu mwovu ana taabu nyingi, bali upendo usio na kikomo wa Bwana unamzunguka mtu anayemtumaini.
Many are the sorrows of the wicked; but he that trusteth in the LORD, mercy compasseth him about.
11 Shangilieni katika Bwana na mfurahi, enyi wenye haki! Imbeni, nyote mlio wanyofu wa moyo!
Be glad in the LORD, and rejoice, ye righteous; and shout for joy, all ye that are upright in heart.

< Zaburi 32 >