< Zaburi 30 >
1 Utenzi wa kuweka wakfu hekalu. Zaburi ya Daudi. Nitakutukuza wewe, Ee Bwana, kwa kuwa umeniinua kutoka vilindi, na hukuacha adui zangu washangilie juu yangu.
Psalm Davidov, pesem posvečevanja hiše njegove. Poveličeval te bodem, Gospod, ker si me povzdignil, in sovražnikom mojim nisi dal radovati se nad mano.
2 Ee Bwana, Mungu wangu, nilikuita unisaidie na wewe umeniponya.
Gospod, Bog moj, ko sem vpil do tebe, ozdravil si me.
3 Ee Bwana, umenitoa Kuzimu, umeniokoa nisishuke kwenye shimo la mauti. (Sheol )
Gospod, izpeljal si iz groba dušo mojo, ohranil me živega, da ne idem v grob. (Sheol )
4 Mwimbieni Bwana, enyi watakatifu wake; lisifuni jina lake takatifu.
Prepevajte Gospodu, katerim on deli milost, in slavite spomin svetosti njegove.
5 Kwa maana hasira yake ni ya muda mfupi, bali upendo wake hudumu siku zote. Inawezekana kilio kiwepo usiku kucha, lakini asubuhi kukawa na furaha.
Ko je bil trenotje v jezi svoji, pride življenje po dobroti njegovi; ako se zvečer oglasi jok, zjutraj petje.
6 Nilipofanikiwa nilisema, “Sitatikiswa kamwe.”
Ker jaz sem govoril v mirnosti svoji: Ne omahnem vekomaj.
7 Ee Bwana, uliponijalia, uliuimarisha mlima wangu, lakini ulipouficha uso wako nilifadhaika.
Gospod, po dobroti svoji si bil na goro postavil mojo moč; ko si skrival obličje svoje, bil sem zbegan.
8 Kwako wewe, Ee Bwana, niliita, kwa Bwana niliomba rehema:
K tebi sem klical, Gospod, in Gospoda sem prosil:
9 “Kuna faida gani katika kuangamia kwangu? Katika kushuka kwangu shimoni? Je, mavumbi yatakusifu? Je, yatatangaza uaminifu wako?
Kaj prida bode v krvi moji, ko pojdem dol v jamo? ali te bode prah slavil? bode li oznanjal resnico tvojo?
10 Ee Bwana, unisikie na kunihurumia, Ee Bwana, uwe msaada wangu.”
Čuj, Gospod, in milost mi stórí; Gospod, bodi mi pomočnik.
11 Uligeuza maombolezo yangu kuwa kucheza, ulinivua nguo za gunia ukanivika shangwe,
Izpreobrnil si mi jok moj v ples; razpasal si raševnik moj in opasal me z radostjo:
12 ili moyo wangu uweze kukusifu na usikae kimya. Ee Bwana Mungu wangu, nitakushukuru milele.
Da ti prepeva slava in ne umolkne. Gospod, Bog moj, slavil te bodem vekomaj.