< Zaburi 30 >
1 Utenzi wa kuweka wakfu hekalu. Zaburi ya Daudi. Nitakutukuza wewe, Ee Bwana, kwa kuwa umeniinua kutoka vilindi, na hukuacha adui zangu washangilie juu yangu.
Psalmus cantici, in dedicatione domus David. [Exaltabo te, Domine, quoniam suscepisti me, nec delectasti inimicos meos super me.
2 Ee Bwana, Mungu wangu, nilikuita unisaidie na wewe umeniponya.
Domine Deus meus, clamavi ad te, et sanasti me.
3 Ee Bwana, umenitoa Kuzimu, umeniokoa nisishuke kwenye shimo la mauti. (Sheol )
Domine, eduxisti ab inferno animam meam; salvasti me a descendentibus in lacum. (Sheol )
4 Mwimbieni Bwana, enyi watakatifu wake; lisifuni jina lake takatifu.
Psallite Domino, sancti ejus; et confitemini memoriæ sanctitatis ejus.
5 Kwa maana hasira yake ni ya muda mfupi, bali upendo wake hudumu siku zote. Inawezekana kilio kiwepo usiku kucha, lakini asubuhi kukawa na furaha.
Quoniam ira in indignatione ejus, et vita in voluntate ejus: ad vesperum demorabitur fletus, et ad matutinum lætitia.
6 Nilipofanikiwa nilisema, “Sitatikiswa kamwe.”
Ego autem dixi in abundantia mea: Non movebor in æternum.
7 Ee Bwana, uliponijalia, uliuimarisha mlima wangu, lakini ulipouficha uso wako nilifadhaika.
Domine, in voluntate tua præstitisti decori meo virtutem; avertisti faciem tuam a me, et factus sum conturbatus.
8 Kwako wewe, Ee Bwana, niliita, kwa Bwana niliomba rehema:
Ad te, Domine, clamabo, et ad Deum meum deprecabor.
9 “Kuna faida gani katika kuangamia kwangu? Katika kushuka kwangu shimoni? Je, mavumbi yatakusifu? Je, yatatangaza uaminifu wako?
Quæ utilitas in sanguine meo, dum descendo in corruptionem? numquid confitebitur tibi pulvis, aut annuntiabit veritatem tuam?
10 Ee Bwana, unisikie na kunihurumia, Ee Bwana, uwe msaada wangu.”
Audivit Dominus, et misertus est mei; Dominus factus est adjutor meus.
11 Uligeuza maombolezo yangu kuwa kucheza, ulinivua nguo za gunia ukanivika shangwe,
Convertisti planctum meum in gaudium mihi; conscidisti saccum meum, et circumdedisti me lætitia:
12 ili moyo wangu uweze kukusifu na usikae kimya. Ee Bwana Mungu wangu, nitakushukuru milele.
ut cantet tibi gloria mea, et non compungar. Domine Deus meus, in æternum confitebor tibi.]