< Zaburi 30 >

1 Utenzi wa kuweka wakfu hekalu. Zaburi ya Daudi. Nitakutukuza wewe, Ee Bwana, kwa kuwa umeniinua kutoka vilindi, na hukuacha adui zangu washangilie juu yangu.
Psaume. Cantique pour la dédicace de la maison. De David. Je t’exalte, Yahweh, car tu m’as relevé, tu n’as pas réjoui mes ennemis à mon sujet.
2 Ee Bwana, Mungu wangu, nilikuita unisaidie na wewe umeniponya.
Yahweh, mon Dieu, j’ai crié vers toi, et tu m’as guéri.
3 Ee Bwana, umenitoa Kuzimu, umeniokoa nisishuke kwenye shimo la mauti. (Sheol h7585)
Yahweh, tu as fait remonter mon âme du schéol, tu m’as rendu la vie, loin de ceux qui descendent dans la fosse. (Sheol h7585)
4 Mwimbieni Bwana, enyi watakatifu wake; lisifuni jina lake takatifu.
Chantez Yahweh, vous ses fidèles, célébrez son saint souvenir!
5 Kwa maana hasira yake ni ya muda mfupi, bali upendo wake hudumu siku zote. Inawezekana kilio kiwepo usiku kucha, lakini asubuhi kukawa na furaha.
Car sa colère dure un instant, mais sa grâce toute la vie; le soir viennent les pleurs, et le matin l’allégresse.
6 Nilipofanikiwa nilisema, “Sitatikiswa kamwe.”
Je disais dans ma sécurité: « Je ne serai jamais ébranlé! »
7 Ee Bwana, uliponijalia, uliuimarisha mlima wangu, lakini ulipouficha uso wako nilifadhaika.
Yahweh, par ta grâce, tu avais affermi ma montagne; — tu as caché ta face, et j’ai été troublé.
8 Kwako wewe, Ee Bwana, niliita, kwa Bwana niliomba rehema:
Yahweh, j’ai crié vers toi, j’ai imploré Yahweh:
9 “Kuna faida gani katika kuangamia kwangu? Katika kushuka kwangu shimoni? Je, mavumbi yatakusifu? Je, yatatangaza uaminifu wako?
« Que gagnes-tu à verser mon sang; à me faire descendre dans la fosse? La poussière chantera-t-elle tes louanges, annoncera-t-elle ta vérité?
10 Ee Bwana, unisikie na kunihurumia, Ee Bwana, uwe msaada wangu.”
Ecoute, Yahweh, sois-moi propice; Yahweh, viens à mon secours! » —
11 Uligeuza maombolezo yangu kuwa kucheza, ulinivua nguo za gunia ukanivika shangwe,
Et tu as changé mes lamentations en allégresse, tu as délié mon sac et tu m’as ceint de joie,
12 ili moyo wangu uweze kukusifu na usikae kimya. Ee Bwana Mungu wangu, nitakushukuru milele.
afin que mon âme te chante et ne se taise pas. Yahweh, mon Dieu, à jamais je te louerai.

< Zaburi 30 >