< Zaburi 30 >
1 Utenzi wa kuweka wakfu hekalu. Zaburi ya Daudi. Nitakutukuza wewe, Ee Bwana, kwa kuwa umeniinua kutoka vilindi, na hukuacha adui zangu washangilie juu yangu.
A psalm of David. A song for the dedication of the Temple. I will extol you, O Lord, because you have lifted me up, and not suffered my foes to rejoice over me.
2 Ee Bwana, Mungu wangu, nilikuita unisaidie na wewe umeniponya.
I cried to you for help, O Lord my God, and you healed me.
3 Ee Bwana, umenitoa Kuzimu, umeniokoa nisishuke kwenye shimo la mauti. (Sheol )
You have brought me up, Lord, from Sheol, from my way to the pit back to life you have called me. (Sheol )
4 Mwimbieni Bwana, enyi watakatifu wake; lisifuni jina lake takatifu.
Sing praise to the Lord, faithful people; give thanks to his holy name.
5 Kwa maana hasira yake ni ya muda mfupi, bali upendo wake hudumu siku zote. Inawezekana kilio kiwepo usiku kucha, lakini asubuhi kukawa na furaha.
For his anger lasts only a moment, his favor endures for a lifetime. Weeping may lodge for the night, but the morning brings shouts of joy.
6 Nilipofanikiwa nilisema, “Sitatikiswa kamwe.”
When all went well, I imagined that never should I be shaken.
7 Ee Bwana, uliponijalia, uliuimarisha mlima wangu, lakini ulipouficha uso wako nilifadhaika.
For by your favor, O Lord, you had set me on mountains strong: but you hide your face, and I was confounded.
8 Kwako wewe, Ee Bwana, niliita, kwa Bwana niliomba rehema:
Then to you, Lord, I cried, to the Lord I begged for mercy,
9 “Kuna faida gani katika kuangamia kwangu? Katika kushuka kwangu shimoni? Je, mavumbi yatakusifu? Je, yatatangaza uaminifu wako?
“What profit is there in my blood, if I go down to the pit? Can you be praised by dust? Can it tell of your faithfulness?
10 Ee Bwana, unisikie na kunihurumia, Ee Bwana, uwe msaada wangu.”
Hear, Lord, and show me your favor, Lord be a helper to me.”
11 Uligeuza maombolezo yangu kuwa kucheza, ulinivua nguo za gunia ukanivika shangwe,
You have turned my mourning to dancing; my sackcloth you have unloosed, and clothed me with joy:
12 ili moyo wangu uweze kukusifu na usikae kimya. Ee Bwana Mungu wangu, nitakushukuru milele.
that unceasingly I should sing your praise, and give thanks to you, Lord my God, forever.